Monday, June 8, 2015

MABINGWA wa kandanda Tanzania bara, Young Africans kesho wanatarajia kuanza maandalizi ya ligi kuu msimu ujao pamoja na kombe la Kagame linalotarajia kuanza kutimua vumbi jijini Dar es salaam Julai 11 mwaka huu.
Katibu mkuu wa Yanga, Dr. Jonas Tiboroha amesema mazoezi hayo yatakuwa yanafanyika uwanja wa Karume, Ilala, Dar es salaam chini ya kocha mkuu, Mholanzi, Hans van der Pluijm aliyetua Dar usiku wa kuamkia leo akitokea kwake nchini Ghana.

“Kazi imeanza, kesho asubuhi mazoezi ya kwanza yanaanza Karume, tunaanza pole pole kwasababu wachezaji wetu wengi wapo timu za taifa zote mbili”. Amesema Dr. Tiboroha na kuongeza: “Wachezaji wengine wa kimataifa kama Tambwe (Amiss), Niyonzima (Haruna) wapo kwenye timu zao za taifa, lakini wachezaji wengine kama Kpah Sherman watawasili kesho, ila wengi watawasili tarehe 16”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video