Monday, June 1, 2015

Na Ramadhani Ngoda.
Kiungo wa FC Barcelona anayetazamiwa kuiacha klabu hiyo, Xavi Hernadez amekanusha vikali uwezekano wa yeye kujiunga na mabingwa wa Ufaransa PSG baada ya kumaliza muda wake katika miamba hiyo ya Hispania.
Xavi ambaye anatazamiwa kucheza mchezo wa mwisho akiwa na Barcelona katika mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Juventus katika uwanja uwanja wa Berlin, amewekanusha taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari nchini Ufaransa kuwa anaweza kujiunga na PSG kwa mkopo kabla kutimkia katika klabu ya Al Sadd ya Qatar aliyoingia nayo mkataba wa miaka miwili.


“Sitaichezea PSG,” Xavi aliliambiwa gazeti la Al-watan la nchini Qatar.

Habari za kiungo huyo kujiunga na PSG zilitiwa nguvu na ukweli kuwa mmiliki wa klabu hiyo ni kaka wa mwenyekiti wa PSG Nasser Al-Khelaifi.

Xavi aliisaidia Barcelona kutwaa ubingwa wa Copa Del Rey waliposhinda 3-1 dhidi ya Athletic Bilbao katika mchezo wa fainali jumamosi iliyopita.

Kama Barcelona watafanikiwa kuifunga Juventus katika mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa siku ya Jumamosi, itakuwa ni taji la 4 kwa veteran huyo akiwa na Barcelona kwani mpaka sasa tayari amekwishinda mataji matatu ya ligi hiyo.

Xavi amefikia uamuzi wa kuachana na Bacelona baada ya kuitumikia kwa takriban maisha yake yote ya soka na kufanikiwa kushinda mataji nane ya La Liga na matatu ya Copa Del Rey.



0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video