Monday, June 8, 2015


Na Ramadhani Ngoda

Miaka 19 ya Mfaransa Arsene Wenger katika klabu ya Arsenal ni sawa na ‘chungu tamu’  maana ina mazuri na mabaya ya kuhadithia kwa wapenzi wa klabu hiyo yenye maskani yake Kaskazini mwa jiji la London.

Tangu kuwasili kwake Higbury (wakati huo) mnamo mwaka 1996, ni wazi kuwa amefanya makubwa yanayostahili chungu ya shukrani kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Moja ikiwa ni kuipa Arsenal mataji matatu ya ligi kuu mpaka sasa akifuta ukame wa miaka 7 bila taji la ligi kwani taji la mwisho kwa Arsenal lilikuwa ni msimu wa 1990/91 chini ya George Graham kabla ya Wenger kurudisha heshima hiyo msimu wa 1997/98 na kushinda mengine miaka ya 2002 na lile la 2003/04.

Arsenal akishangilia ubingwa wa ligi kuu Uingereza msimu wa 1997/98

Ni kweli walivyonena waswahili, ‘mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.’ Kubwa jingine linaloweza kuwa dhahabu ya Wenger kwa wana Arsenal, ni mataji 6 ya kombe la FA chini ya uongozi wake katika klabu hiyo. Ikumbukwe kuwa hakuna kocha aliyewahi kuchukua hata mataji mawili ya kombe hilo tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo miaka 129 iliyopita kuanzia Thomas Mitchell hadi Pat Rice aliyekabidhi kijiti kwa Wenger. Hongera ‘profesa’ kwa hili.

Lakini kama hiyo haitoshi, Arsenal watakumbuka medali za mshindi wa pili walizovaa mwaka 2006 japo waliusaliti ubingwa huo kwa wababe wa Hispania FC Barcelona. Fainali iliyodhihirisha kweli ‘la kuvunda halina ubani’ kwani ilikuwa ni nafasi pekee ya Arsenal kutwaa kwa mara ya kwanza taji hilo kutokana na ukweli kuwa mashabiki, wachezaji pamoja na makocha waliowahi kuinoa Arsenal, hawajui ladha ya taji hilo kubwa barani barani Ulaya. Lakini kwa walichoambulia si haba.

‘Utamu wa muwa ni fundo.’ Mzee Wenger ni lazima akiri kuwa ana madeni kwa wana Arsenal ambayo pengine kuyalipa kabla hajajafikia ukomo wa maisha yake Emirates ni jambo bora na la kihistoria litakalomfanya akumbukwe Zaidi klabuni hapo.

Kubwa la madeni mengi aliyonayo, ni kuipa Arsenal kitu wanachokishuhudia tu kwa vilabu vingine kama FC Barcelona, Real Madrid, Bayern Munich, Manchester United, Liverpool na nyingine nyingi barani Ulaya. Na hili si jingine bali ni Ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Arsene Wenger baada ya fainali ya ligi ya mabingwa msimu wa 2005/06 dhidi ya FC Barcelona na kuambulia nafasi ya pili

Kuhama kutoka uwanja wa zamani wa Highbury kwenda Emirates, kumekuwa kukitajwa kama kichocheo kikubwa cha Arsenal kushindwa kusajili wachezaji wenye majina makubwa kama tunavyowaona sasa na wengine wakizidi kutajwa. Hii ni ishara kuwa, sasa mzee Wenger atakuwa hana kisingizio kwani anapewa donge kubwa la usajili ili kujenga kikosi chenye ushindani kitakacholeta ‘champions league’ katika uwanja wa Emirates.

Alexis Sanchez, Mesut Ozil, David Ospina na Mathew Debuchy wanaonekana kuwa mwanzo tu wa ujio wa majina mengi makubwa katika klabu hiyo kama walivyokwisha taja wakiana Arturo Vidal, Morgan Schdeiderlin, Edinson na wengine. Lipo linalotafutwa bila shaka. Wenger lipa deni hili kwa watu waliokuvumilia kwa Zaidi ya miaka 10 uliyoboronga.

Deni la pili linaweza kuwa taji la ligi kuu nchini humo ambalo licha ya kuvunja ukame wake mwaka 1998 (mwaka wa pili baada ya kuichukue Arsenal), taji hilo limekuwa adimu Zaidi ya nyota ya jaha kwa wapenzi wa klabu hiyo kwani hawajaliona sura yake tangu mwaka 2004 walipochukua kwa mara ya mwisho.


Ukiacha ukweli kuwa, taji la FA walilotwaa msimu wa 2013/14, ni taji lililofuta vumbi kabati la mataji ya klabu hiyo kwa miaka 10, bado wanazi hao wana kiu ya miaka 11 ya taji la ligi kuu nchini humo. Bila shaka wanaumia na kuchoshwa na kuziona Manchester city, Manchester United na Chelsea wakipokezana ubingwa huo kama mbio za vijiti. Wenger inambidi kutengeneza chemchem ya maji itakayokata kiu hii ya Zaidi ya muongo mmoja sasa.


Bila shaka anatakiwa kwa namna moja au nyingine kutilia maanani maneno ya wakongwe wa klabu hiyo, wakina Robert Pires, Patrick  Vieira, Rey Parlour na wengine waliowahi kumshauri aongeze wachezaji wenye uwezo mkubwa wanaoweza kushindana ndani ya Uingereza lakini pia barani Ulaya. Bila shaka hawa walitaka kuwaona wakina Sanchez na Ozil wengi wakisajiliwa Arsenal. Na hili ndio linaloonekana kuwa katika akili za wana Arsenal wengi duniani kote.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video