Tuesday, June 9, 2015

Lowassa ni miongoni mwa makada wa CCM waliotangaza nia na alisema ataboresha michezo ingawa hakuanisha sera madhubuti

WAKATI vuguvugu la watu kutangaza nia ya kuomba kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) likiendelea, Rais wa kampuni ya ngumi za kulipwa nchini, TPBO, Yassin Abdallah ‘Ustadh’ amewashukia makada wa chama tawala kwa kushindwa kueleza sera madhubuti juu ya kuendele za michezo nchini.
Yassin amesema kwamba amewasikiliza Watangaza nia wote na kuona wanagusiagusia tu michezo hususani soka, lakini wamesahau michezo mingine isiyokuwa na udhamini mfano Ngumi.
“Watangaza nia wote ni waelezaji wazuri sana kwa maana ya medani ya kisiasa, lakini bado suala la michezo wanagusiagusia tu, hakuna ambaye amezungumza kiundani ni vitu gani atawafanyia Watanzania kwenye michezo. Ukiangalia wote wanazungumzia soka, kwani Tanzania ni nchi ya mpira wa miguu tu? Kuna michezo mingi ambayo haina udhamini kama ngumi, riadha, tenisi, mpira wa kikapu nk”. Amesema Yassin .

 “Sijaona mtu akizungumza kiundani kuhusu michezo, wengine wanasema Wataifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, wanasahau kuwa michezo ni kiwanda cha kutengeneza ajira, wapo watu wengi wanalipwa mabilioni kwenye michezo. Maneno yao mimi naona ni siasa tu, ukiangalia viwanja vingi kwasasa vimejaa Diwani Cup, Mbunge Cup, lengo ni kuwashawishi wapiga kura tu, baada ya uchaguzi hakuna jipya”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video