Wednesday, June 10, 2015

Singano aliyepiga magoti kusujudu bado anaipenda Simba

MASHABIKI wa Yanga jana walifurika uwanja wa Karume kushuhudia mazoezi ya timu yao, lakini walipomuona Ramadhan Singano ‘Messi’ akiingia kwenye Ofsi za Shirikisho la soka Tanzania jana akiwa na gari aina ya Mazda kwa ajili ya kikao cha kujadili utata wa mkataba wake na klabu ya Simba, walimshangalia na baadaye kuchangishana pesa walizompatia wakijigamba kuwa Simba haina hela za kumpa, hivyo ajiunge na Yanga.

Ulikuwa utani wa jadi, lakini kitendo hicho kimetafsiriwa tofauti na wadau wengi na kumezuka tetesi kuwa kiungo huyo mshambaliaji amejiunga na mabingwa wa Tanzania bara, Young Africans.

Kutokana na taarifa hizo, Singano amekiri kupokea simu nyingi zikimuuliza kama kweli kajiunga na Yanga, lakini amekanusha uvumi huo.


Kupitia kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook unaokwenda kwa jina la Ramadhan Singano Messi amekanusa taarifa hizo na ameandika hivi:



Nimepokea cm nying sana wakiwa wananiuliza km ni kweli nimejiunga yanga,ila mm nasema siyo kweli na sina mpango huo mm bado naipenda simba

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video