Wednesday, June 10, 2015

Kiungo mkongwe na mahiri wa mabingwa wa soka nchini Italia Juventus, Andrea Pirlo anatarajia kukutana na maofisa wa klabu ya soka ya Sidney,  huku mwakilishi wa klabu hiyo akijaribu kumshawishi kutua nchini Australia na kuachana na mpango wa kujiunga na New York City inayoshiriki ligi ya soka nchini Marekani.
Kiungo huyo mwenye miaka 36 hivi sasa, amepata kuiwakilisha timu yake ya taifa mara 113.

Pirlo ambaye alishindwa kuisaidia timu yake kutamba mbele ya Barcelona katika mchezo wa fainali ya klabu bingwa Ulaya jumamosi iliyopita wakichapwa mabao 3-1, anahusishwa na kuihama klabu yake ya Juventus baada ya kubakiwa na msimu mmoja tu katika mkataba wake.

Pamoja na kuenea kwa taarifa za kiungo huyo kuhamia klabu anayoichezea kiungo wa zamani wa Chelsea na timu ya taifa ya Uingereza,  Frank Lampard, New York City ya nchini Marekani,  lakini mmoja wa mawakala wa klabu ya Sidney ya nchini Australia amekaririwa akisema wanamhitaji mchezaji huyo kwa udi na uvumba.

“kazi yangu ni moja tu hapa nchini Italia. Kama Pirlo ataondoka hapa Turin, basi nitamshawishi ajiunge na timu yetu ya Sidney” alisema afisa huyo na mwakalishi wa klabu hiyo.


Wakala huyo aitwaye Lou Sticca amethibitisha kuwa Sidney inahitaji mchezaji mkubwa ili azibe mapengo yaliyoachwa wazi na wachezaji kadhaa nyota walioihama klabu hiyo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video