Monday, June 1, 2015


Na Dickson Masanja

Mwezi Mei ambao umemalizika jana, Tanzania tulitia aibu kwenye anga la michezo haijawahi kutokea, si kwenye soka, ndondi hata kikapu. Mwezi Mei mwaka huu ulikuwa ni mbaya sana kwa wanamichezo na wapenzi wote wa michezo kwa kile kilichotokea ndani na nje ya mipaka ya nchini yetu kutokana na timu zetu kuboronga kwenye michezo.

Tukianza na soka ambao ndio mchezo wenye mashabiki wengi na unaoongoza kwa kupendwa duniani kote. Mwezi Mei timu yetu ilienda Afrika Kusini kwa ajili ya kushiriki mashindano ya COSAFA baada ya kupewa mwaliko wa kushiriki michuano hiyo inayoshirikisha nchi za ukanda wa Kusini mwa Afrika.

Kitu cha kusikitisha ni kwamba, timu yetu ya Taifa ‘Taifa Stars’ ilipoteza michezo yote mitatu kwenye kundi lake kulikokuwa na timu za Swaziland, Lesotho, Madagascar na kibonde Tanzania. Kibaya zaidi Stars haikufunga hata goli moja kwenye michuano hiyo, baada ya kupigwa mechi zote timu ilirejea nyumbani na sasa inajiandaa kwa ajili ya kufuzu kucheza michuano ya CHAN pamoja na AFCON.

Wapenzi wa soka walikasirishwa sana na matokeo ya Stars huko Afrika Kusini na wengine kudiliki kusema kocha afukuzwe akiwa hukohuko ili akifika hapa achukue kilicho chake na kurejea kwao. Sawa hayo ni maoni na mitazamo ya mashabiki wa soka na pengingine ni kutokana na machungu ya kufungwa na timu ambazo zipo chini sana kwenye viwango vya soka vya FIFA.

Lakini swali langu mimi ni je, kufukuza na kuajiri makocha wapya ni mwarobaini wa tatizo letu? Pasina shaka jibu ni hapana. Basi kama jibu ni hapana sasa tutafute mwarobaini wa tatizo letu. Tatizo linalotutafuna Tanzania ni mfumo mzima wa soka letu, kuanzia uongozi, vilabu, wachezaji mpaka mashabiki.

Kila uongozi mpya uingiapo madarakani huja na sera mpya pamoja na mipango mipya, bila kuangalia sera na mipango ya uongozi uliopita, uongozi ulioingia madarakani huanza upya utekelezaji wa sera na mipango yake. Lakini ikumbukwe inawezekana ilikuwepo mipango mizuri na inayotekelezeka iliyoachwa na uongozi ulioondoka madarakani, lakini walioingia huitupa kule na kuanza upya.

Badala ya kuendeleza yale mazuri yaliyoachwa wanataka kuanza upya ili wasionekane kama wanatekeleza sera za waliopita, huo ni ushamba. Nani kakwambia ukiendeleza kitu kizuri kilichofanywa na mwezio ni vibaya? Hapa ndipo uongozi wetu huanza kupoteza mwelekeo kwa kutaka kuanza upya kila kitu, wakati mwingine hata vitu ambavyo si vya lazima.

Jambo lingine ni urafiki, undugu, kujuana na uswahiba kwenye kazi, viongozi wanapoingia madarakani hutaka kufanya kazi na watu wa karibu yao bila kuangalia uwezo wa utendaji wa mtu husika. Sikatazi kumuweka rafiki wala nduguyo kwenye nafasi fulani, kikubwa tuangalie uwezo wake na nafasi anayopewa kama anaweza kuimudu. Mara nyingi inapotokea ndugu au rafiki wa kiongozi wa mpira anaonekana dhahiri kushindwa kumudu nafasi yake bado huendelea kubebwa na kukumbatiwa.

Vilabu vyetu navyo vimekuwa vikiwajaza ujinga baadhi ya wachezaji, hasa vilabu vyenye nguvu ya kifedha. Hapa namaanisha wachezaji wanapokuwa kwenye vilabu hivi wanaaminishwa kwamba wao ndio kilakitu ‘lulu’ za Tanzania, lakini kumbe kuna wachezaji wengine ni wakali kuliko wao na wapo kwenye vilabu ambavyo havina majina makubwa.

Leo hii Busungu, Mandawa wanapiga magoli zaidi ya 10 lakini nani anatambua hilo. Kuna wachezaji wangapi wanacheza nafasi moja na wachezaji hawa kutoka vilabu hivi vyenye nguvu kifedha lanikini hawajafikisha magoli kama hayo? Lakini wanajiona wao ndio akina Rooney, Ronaldo au Messi kwasababu ndio wameaminishwa hivyo na klabu zao.

Lakini leo wachezaji kama hawa (Mandawa, Busungu na wengine) kuitwa kwenye timu ya Taifa mpaka watu wapige debe kama kama wale wapigadebe wa pale Buguruni-Sheli, hapo utajua ni kwa jinsi gani hivi vilabu vyenye nguvu vina athiri soka la bongo. Mchezaji anaitwa timu ya Taifa kwasababu yupo timu fulani na mwingine haitwi kwasababu yupo timu ile.

Ndio maana wachezaji wengi wakifika kwenye vilabu hivyo wanajiona wamemaliza safari zao za mafanikio na kubweteka, wakati mwingine hutokea hata wakiletewa ofa kutoka vilabu vya nje wanakataa kwenda wakati huohuo wakifungwa utasikia wachezaji walikuwa hawajalipwa mishahara. Sasa unapata wapi ujasiri wa kukataa timu inayokuhitaji wakati hapo ulipo hata mshahara wa mwezi unalipwa kwa manati?

Tuachane na hao twende kwa wachezaji wenyewe, kiukweli malengo ni kitu kizuri sana maishani. Kuma unaishi halafu huna malengo ni bora ungeendelea kubaki mtoto miaka yote. Kwenye malengo kuna malengo ya muda mfupi na yale ya muda mrefu, kama leo ukiniuliza nimefikia wapi kuhusu malengo yangu niliyojiwekea naweza kukupangia yale yaliyotimia na ambayo hayajaimia kwasababu nina malengo.

Wachezaji wa bongo sasa, wanacheza soka ili mradi maisha yanaenda. Hawana malengo kabisa, wanafurahia kuonekana live kwenye TV ili wawe maarufu basi miaka isonge mbele. Au wengingine malengo yao ni kucheza kwenye hivi vilabu vyetu vikongwe basi. Sina maana mbaya hapa ila wengi wanapofika hapo ndo wale niliokwambia wanaanza kujiona akina Rooney, Ronaldo au Messi na hii ni kutokana na kutokuwa na malengo.

Mfano mzuri hapa ni Mbwana Samatta, huyu jamaa anaonekana anajitambua na uwezo wa soka anaounesha uwanjani ni sawa na uwezo wa akili yake kichwani. Sitaki kukwambia Samatta ametokea wapi mpaka sasa hivi anacheza TP Mazembe, jiulize mwenyewe amekaa kwa muda gani pale Msimbazi na akaonekana anajua akanyakuliwa. Huyu jamaa anamalengo ndiyo maana hata pale Mazembe anaona bado hajafika hivyo anajituma zaidi ili asonge mbele zaidi kutimiza malengo yake.

Samatta amewakuta wachezaji wangapi pale Simba na akaondoka akawaacha? Anamalengo ndio maana anapota nafasi aitumia kwa kujituma ili siku moja ndoto zake na malengo aliyojiwekea yatimie.

Sasa hawa wachezaji wasiojielewa na wasio na malengo wanaathiri vipi timu ya Taifa, kwanza kucheza kwenye hivyo vilabu vyenye nguvu kunawapa kiburi wajione wao ni ‘mafaza’ kitu kinachowafanya wasijitume kuanzia kwenye mazoezi mpaka kwenye mechi. Kitu kingine wanajua kabisa ‘piga ua garagaza’ lazima niitwe kwenye timu ya Taifa na lazima nicheze tena kikosi cha kwanza.

Mchezaji kujiona yeye yupo juu ya timu ni kuliua soka letu, kila mchezaji anapaswa kujua umuhimu na wajibu wake kwenye timu ya Taifa, unapopewa nafasi ya kucheza kwenye timu ya Taifa hebu tushawishi tuone ni kwa kiasi gani unastahili kutuwakisha sisi kwenye timu yetu maana ndiyo timu pekee inayotuweka kwenye jukwaa moja.


Sasa kwa hali hiyo unataka tubadishe kocha, sawa tutamleta mwingine nay eye akivurunda tunamleta mwingine halafu mwisho wa siku inakuwaje? Hivi kwani tangu tumeanza kuajiri makocha wa kigeni ni kocha gani ambaye ametupa mafanikio zaidi ya Arcio Maximo kuipeleka Tanzania kwenye mivhuano ya CHAN, tukamfukuza wakaja wengine na tunaendelea kuwafukuza.

Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu, kauli hii aliitoa Rais wa awamu ya pili mzee Ally Hassan Mwinyi akimaanisha hata wale watu wasiojua kunyoa ndio sehemu wanayojifunia kunyoa.  Sasa kwa hayo niliyoyaoodhesha hapo juu tutaendelea kunyolewa tu.

Kwenye makala ijayo, nitakuletea mwendelezo wa aibu nyingine kwenye michezo iliyotokea mwezi Mei, hii itakuwa ni kwenye mpira wa kikapu na masumbwi.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video