Monday, June 8, 2015

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Simba na sasa JKT Ruvu, Betram Mwombeki ameamua kuachana na soka na kurejea kwenye fani yake ya zamani ya uvuvi na ufugaji.
Mwombe amekaririwa na E-fm usiku huu akisema kwasasa yuko Mwanza kwa mapumziko na muda si mrefu anaanza shughuli za ya kufuga na kuvua samaki kwasababu anasumbuliwa sana na miguu inayomuuma kwenye unyayo.
“Niko Mwanza sasa hivi, nimeamua kuachana na mpira kwasababu naumwa miguu kwa chini, kama nachomwa sindano vile. Ilianza niliposajiliwa JKT Ruvu, lakini nikiwa Simba haikuwa kunitokea”. Amesema Mwombeki na kuongeza: “Nimeamua kurudi kwenye fani yangu ya zamani ya ufugaji na uvuvi”.

Mwamboki amebakiza mkataba wa mwaka mmoja katika klabu yake ya JKT Ruvu, lakini anaamini watamalizana bila matatizo yoyote.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video