Tuesday, June 2, 2015

WEKUNDU wa Msimba Simba wanajiandaa kumchukulia hatua za kisheria mshambuliaji wao mahiri, Ramadhani Singano ‘Messi’ kwa kuituhumu klabu hiyo kughushi mkataba wake.


Afisa habari wa Simba, Hajji Manara amewaambia waandishi wa habari leo makao makuu ya klabu, Msimbazi, Kariakoo, Dar es salaam kwamba , Simba haijaghushi mkataba wa Singano kama anavyodai yeye na meneja wake Hamis Ramadhan ambaye ni kaka yake wa damu, lakini kwasasa ndiye msimamizi wake.  

“Simba inatambua mkataba wa Messi unamalizika mwakani na si mwaka huu kama anavyodai. Kama kuna klabu inamuhitaji mchezaji huyo, bora ijitokeze na kufanya mazungumzo ramsi na Simba,”amesema Manara na kusisitiza:  “Kitendo alichokifanya Messi kinafanyiwa kazi na mamlaka za ndani za Simba na baadaye tutatoa tamko la hatua tuliyochukua,”.

Siku za karibuni, Singano ameishutumu klabu yake kwa kughushi mkataba wake akidai kuwa mkataba wake halali ni wa miaka miwili aliosaini Mei mosi mwaka 2013 na unatakiwa kumalizika Julai 1 mwaka huu.

Simba wao wana mkataba wa miaka mitatu uliosainiwa mei 1, 2013 na utamalizika Julai 1, 2016.

Wakati hayo yakiendelea tayari Simba walishatengeneza mkataba mwingine wa Messi uliotakiwa kusainiwa juni 1 mwaka huu, lakini nyota huyo aligoma akishinikiza kwanza tatizo la mkataba wake wa kwanza lipatiwe ufumbuzi, halafu mkataba mpya urekebishwe baadhi ya vipengele.


Hata katika mkataba wa kwanza, Messi anadai kuna vipengele havijatimizwa mathalani kulipiwa kodi ya nyumba.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video