MSHAMBULIAJI machachari wa Liverpool, Raheem Sterling
huenda akaelekea katika klabu ya Manchester United , ingawa nyota huyo mwenye
umri wa miaka 20 ana wasiwasi kuhusu athari za uhamisho huo kutokana na
ushindani mkali uliopo kati ya klabu hizo mbili.
Unite ikihaha kuinasa saini ya Sterling,
tayari Liverpool imesema haiko tayari kufanya biashara na wapinzani wao wakuu
kutoka Kaskazini Magharibi.
Mkufunzi wa klabu ya Manchester United, Luois Van Gaal anavutiwa na kasi ya uchezaji ya
mchezaji huyo na uwezo wake wa kuwachachafya mabeki.
Sterling amekataa kusaini mkataba mpya Liverpool
ambao atalipwa mshahara wa paundi laki moja kwa wiki akisema kuwa anataka
kuondoka na kuichezea klabu ambayo ina uwezo wa kushinda mataji pamoja na
kushiriki Uefa Champions League msimu ujao.
0 comments:
Post a Comment