Monday, June 1, 2015

Na Ramadhani Ngoda,
Licha ya baadhi ya wanazi wa Arsenal kufurahishwa na tetesi za kutua Emirates kwa winga wa Liverpool Raheem Sterling, veterani wa klabu hiyo, Rey Parlour meibuka na kukandia suala la kumuhitaji mchezaji huyo.

Kumekuwepo na tetesi za Arsenal na Liverpool kubadilishana wachezaji Raheem Sterling na Theo Walcott na kuibua mjadala mkubwa juu ya sakata hilo.

Licha ya tetesi hizo, kiungo huyo wa zamani wa Arsenal haoni ujio wa Sterling kama una manufaa na faida kwa timu hiyo ya Kaskazini mwa London.


Parlour anaona Arsenal wanahitaji kufanya marekebisho katika nafasi mbalimbali kama kiungo wa kati, beki na mshambuliaji wa kati lakini sio Raheem Sterling.

“Ningejikita Zaidi katika kiungo wa kati, beki wa kati, mshambuliaji au golikipa kama ningekuwa kocha,” alisema Palour.

Uwezekano wa dili la kubadilishana wacheaji hao huenda pia likakwamishwa na kiwango alichoonesha Walcott katika mchezo dhidi ya Westbrom aliopachika mabao matatu lakini pia akifunga bao moja kati manne katika mchezo wa fainali ya kombe la FA dhidi ya Aston Villa.

Arsenal wanaonekana kuwa katika mawindo ya wachezaji mbalimbali katika kuboresha kikosi chake wakiwemo Karim Benzema(Real Madrid), Arturo Vidal(Juventus), Edinson Cavani(PSG) na Arsene Wenger analazimika kuingia mfukoni ili kukamilisha sajili hizo.
Kitendo cha Madrid kubadili mfumo katika safu yake ya ushambuliaji kwa kumuweka Gareth Bale kama mshambuliaji wa kati kunaweza kuchagiza upatikanaji wa mshambuliaji Karim Benzema anayeonekana kuwa mbali na mipango ya kocha Rafa Benitez.

Hali ya uchumi ya washika bunduki hao katika miaka ya hivi karibuni pia inaongeza uwezekana wa kuona sura mpya nyingi katika klabu hiyo.

“Hali ya uchumi kwa sasa ni nzuri Zaidi ukilinganisha na ya miaka mitano hadi sita iliyopita. Kuwapata Mesut Ozil na Alexis Sanchez katika kipindi cha miaka michache iliyopita kunaonesha jinsi gani Arsene Wenger hahofii kusajili wachezaji wanaoonekana kuwa na msaada kwa timu,” aliongeza Parlour.

Arsenal waliomaliza nafasi ya tatu nyuma ya mabingwa Chelsea na Manchester City waliomaliza wa pili, wanahitaji kutengeneza kikosi cha ushindani Zaidi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu Uingereza na Ligi ya mabingwa barani Ulaya.







0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video