Tuesday, June 9, 2015

Chidiebele

UONGOZI wa Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’  unahaha kuinasa saini ya mshambuliaji hatari wa Stand United ‘Chama la Wana’, Mnigeria, Abasalim Chidiebele ambaye amemaliza mkataba na klabu yake yenye makazi yake mkoani, Shinyanga.
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Coastal Union, Salim Bawaziri amesema hawataki kukurupuka kwenye suala la usajili na wanasubiri safu mpya ya uongozi itayoingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Julai 5 mwaka huu.
“Mipango ya usajili inaendelea vizuri, unajua usajili una mambo mengi sana, kuna kukaa na wachezaji na kuelewana nao juu ya mikataba yao. Sisi tumetulia na hatutaki kukurupuka, nadhani viongozi watakapopatikana tutaanza rasmi”. Amesema Bawaziri na kuongeza: “ Chidiebele (Abasilim) tunafanya naye mazungumzo, tupo katika hali nzuri, tukimalizana naye tutamtangaza”.
Mbali na Coastal, timu za  Kagera Sugar na Mbeya City fc zipo kwenye windo la kumnasa Chidiebele aliyefunga magoli 11 msimu uliopita wa  ligi kuu uliomalizika Mei 9 mwaka huu kwa Yanga kutawazwa mabingwa wapya wa ligi kuu Tanzania bara.

Chidiebele mwenyewe amethibitisha kuwa kwenye mazungumza na klabu tatu kwa maana ya Kagera, Mbeya City na Coastal, lakini bado hajafikia makubaliano yoyote na amesisitiza kuihama Stand United akidai ina ubabaiuhaji mwingi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video