Tuesday, June 2, 2015

Na Ramadhani Ngoda
Kinara wa mabao katika ligi kuu soka nchini Ufaransa  Alexandre Lacazette amekiri kuwa itakuwa vigumu kwake kuzipiga chini ofa kutoka Barcelona au Real Madrid pindi atakapohitajika na wababe hao wa Hispania na kuzikata maini Manchester City na Liverpool zinazomuwania kwa udi na uvumba katika kipindi hiki cha usajili.

Lacazette(24) ameibuka kinara katika upachikaji mabao nchini humo baada ya kuifungia Olympic Lyon mabao 27 na kuwawezesha mabingwa hao wa zamani wa Ufaransa kushika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Paris Saint Germain (PSG).

Alexandre Lacazette akishangilia moja ya mabao aliyoifungia Olympic Lyon.

Licha ya klabu nyingi kumuhitaji mfumania nyavu huyo, Liverpool na Manchester City zimekuwa viongozi wa riadha ya kupata sahihi yake lakini kauli yake inaonekana kuzivunja moyo klabu hizo za nchini Uingereza.

“Sijafanya maamuzi bado. Lakini ni vigumu kusema hapana kwa Barcelona au Real Madrid japo kwa sasa sifikirii kuhusu hilo,” Lacazetter aliliambia gazeti la ‘Le Parisien’ la Ufaransa.

Hali ya Arsenal kumuhitaji Kareem Benzema inaweza kuwafanya Madrid wahamishie akili kwa Lacazettee na kuua kabisa ndoto za Liverpool ama matajiri wa jiji la Manchester, Manchester City kupata huduma ya mshambuliaji huyo.

Pamoja na hayo, Lacazette amemtupia mzigo wakala wake kujadiliana na timu yoyote inayomuhitaji na yeye atakuwa tayari kwa lolote ambalo wakala wake ataona lina manufaa kwake na hatasita kufanya maamuzi.

“Nitaendelea na likizo yangu, nitamuacha wakala wangu alijadili hili na kujiridhisha. Sitakuwa na wasiwasi nalo,” alisisitiza Lacazette.

Lakini nyota huyo bado hajafuta kabisa uwezekano wa kubaki kwa mabingwa hao mara saba wa  ufaransa kwa msimu mwingine licha ya vilabu kadha wa kadha barani Ulaya kufanya jitihada za kumuondoa ‘Stade De Gerland’ akisisitiza kuwa anaweza kubaki na kuwa na msimu mbaya au mzuri.

“Naweza kubaki Lyon na nikawa na msimu mbaya kama ninavyoweza kuondoka na kuwa namsimu mzuri (aendako). Inategemea na mafikio yangu, kama nakwenda kwenye timu ambayo ina washambuliaji sita, si sawa na hapa nilipo(Lyon) ambapo ni chaguo la kwanza,” aliongeza mpachika mabao huyo.

Alexandre Lacazette aliyelelewa katika kituo cha kukuzia vipaji cha ELCS Lyon na kupandishwa katika timu ya wakubwa  ya Lyon mwaka 2010, ameshaichezea klabu hiyo michezo 139 na kufanikiwa kupachika wavuni mabao 51 ndani ya miaka mitano aliyoitumikia Lyon almaarufu kama ‘The Kids’ inayomilikiwa na mfanya biashara maarufu Jean-Michel Aulas.





0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video