Monday, June 8, 2015

Na Ramadhani Ngoda.
Mlinda lango wa Tottenham Hotspur na timu ya taifa ya Ufaransa, Hugo Lloris ameweka wazi matamanio yake ya kutaka kucheza ligi ya mabingwa barani Ulya na kuzipa nguvu tetesi za yeye kurithi mikoba ya David De gea anayetarajiwa kutimkia Real Mdrid katika kipindi hiki cha usajili.

Lloris (24) ni mmoja kati ya makipa waliounda orodha ya walinda lango wanaohitajika na Man United kuchukua nafasi ya De gea anayeonekana kuwa karibu na mlango wa kutokea Old Trafford na kurejea katika jiji la Madrid.

“Nadhani kila mchezaji anapenda kucheza ligi ya mabingwa kwa sababu ndio kiwango cha juu kabisa, tunatafuta hilo  siku zote. Na naamini nitacheza ligi ya mabingwa tena,” alinena Lloris.


Inafahamika kuwa Lloris ni moja kati ya makipa bora kwa sasa na hii inarandana na ukweli kuwa Mdachi Luis Van Gaal anakuna kichwa kusaka kipa anayeweza kuziba vema pengo la De Gea licha ya kumsajili Victor Valdes kwa mkataba wa miezi 18 kutoka FC Barcelona.

Mfaransa huyo aliyesajiliwa na Spurs kutoka Lyon mwaka 2012 kwa ada ya pauni milioni 8, licha ya shauku ya kucheza ligi ya mabingwa, hatalazimisha kuondoka White Hart Lane kwa sasa kutokana na kuiheshimu klabu yake.

“Nina mkataba mpaka 2019, na ninaheshimu uongozi, klabu pamoja na wachezaji wenzangu hivyo nsingependa kuongelea hilo,” aliongeza Lloris.

Alipoulizwa juu ya uwezekano way eye kumrithi David De gea Man Utd, Lloris alikataa kuweka wazi msimamo wake kutokana na De gea kuwa bado ni mchezaji wa United kwa sasa.

“De gea bado ni mlinda lango wa Manchester United kwa sasa, hivyo sioni haja ya kulizungumzia suala hilo,” alisisitiza Mfaransa huyo.

Hugo Lloris aliyewahi kuzichezea klabu za Nice na Olympic Lyon za Ufaransa kabla kuhamia Uingereza, ameshaichezea Tottenham michezo 100 pamoja na michezo 65 aliyoitumikia timu ya taifa ya Ufaransa katika michuano tofauti tofauti.



  

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video