Mshambuliaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Brazil Marta
Vieira da Silva maarufu kama Marta ameweka historia ya kuwa mfungaji bora wa
michuano ya kombe la dunia la wanawake baada ya kufikisha mabao 15.
Marta wenye umri wa miaka 29, amefikisha idadi ya mabao hayo
baada ya kufunga bao moja kwa mkwaju wa penati kwenye mchezo wa timu yake dhidi
ya korea kusini ambapo Brazili waliibuka kidedea kwa mabao 2-0.
Ushindi huo umeifanya Brazil kuwa vinara wa kundi E, Baada
ya Hispania na Costa Rica kwenda sare ya kufungana 1-1.
Mshambuliaji huyu ameichezea timu ya taifa jumla ya michezo
137 akiwa kafunga mabao 93. Kwa sasa Marta ni mchezaji wa klabu ya Rosengard FC
ya Sweden.
0 comments:
Post a Comment