Wednesday, June 10, 2015


MAMA wa mchezaji nyota wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo ajulikanaye kama Doroles Aveiro alijikuta kwenye utata na vyombo vya usalama katika uwanja wa ndege mjini Madrid mwezi uliopita, imefahamika.

Gazeti la del mundo la nchini Hispania linaripoti kuwa mama huyo mwenye umri wa miaka 60 alikutwa na kitita cha dola 55,000 za kimarekani katika mkoba wake uwanja wa ndege akijiandaa kuruka kwenda kwao nchini Ureno.

Pesa hizo ni kinyume na sheria za wasafiri nchini humo kwani kiwango stahili kwa wasafiri kubeba pesa wanapotoka nje ya nchi ni dola 10,000 tu za marekani.

Inaelezwa kuwa mzazi huyo wa mchezaji bora wa dunia hivi sasa, hakujaza fomu zinazojazwa kueleza sababu za kutoka na pesa zaidi ya dola 10,000 nje ya Hispania.

Watu wa usalama wa kijamii katika uwanja huo wa ndege wakitimiza majukumu yao walimtunzia mama huyo kiasi kilichozidi chote yaani dola 45,000 na kumruhusu aendelee na safari.

Kwa mujibu wa magazeti nchini Hispania, mtu anayekutwa na kosa hilo hutozwa faini isiyopungua dola 600.


Mama huyo ambaye amekua karibu sana na mwanae ‘Ronaldo’ wanaishi pamoja katika jumba la kifahari mjini Madrid nchini Hispania, sambamba na mjukuu wake yaani mtoto wa Cristiano. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video