Wednesday, June 10, 2015

Gwiji la zamani la soka , Diego  Maradona ameibuka na kusema angeweza kuwa makamu wa rais wa shirikisho la soka Ulimwenguni FIFA endapo Prince Ali angeshinda urais.
Prince Ali ndiye alikuwa mpinzani pekee wa Sepp Blatter katika uchaguzi mkuu wa FIFA uliofanyika majuma kadhaa yaliyopita.

 Hata hivyo Blatter alishinda nafasi hiyo ya juu kabisa ya chombo hicho cha mpira wa miguu duniani, ingawa alijiuzulu siku kadhaa baadaye.

Maradona aliyeisaidia timu yake ya taifa ya Argentina kutwaa kombe la dunia mwaka 1986 anaamini alikuwa na nafasi kubwa ya kuwa makamu wa rais wa shirikisho hilo kama Prince Ali angeshinda.

Hata hivyo haijathibitika kama Prince Ali atagombea tena mara uchaguzi utakapofanyika mapema mwakani, lakini uwezekano ni mkubwa kwa raia huyo wa Jordan kugombea.

Blatter ametangaza kuachia ngazi katika shirikisho hilo la soka duniani kutokana na kashfa za rushwa zilizolichafua shirikisho na sura nzima ya mpira wa miguu.


Maradona alikaririwa akiiambia ITV kwamba atalisafisha shirikisho hilo kama akipata nafasi ya kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa chombo hicho.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video