Wednesday, June 10, 2015

KIUNGO mkongwe na nahodha wa zamani wa Taifa Stars,  Henry Joseph Shindika ameonesha nia ya kujiunga na Mwadui FC wakati huu hana timu yoyote tangu amalize mkataba  Mtibwa Sugar msimu uliopia.

Henry aliyewahi kutamba na Simba SC miaka ya nyuma kabla ya kutimkia Kongsvinger ya Norway, amemalizana na Mtibwa katika msimu uliomalizika hivi karibuni na yupo huru kutua popote lakini ameanza kwa kuitaja Mwadui iliyopanda kushiriki Ligi Kuu Bara msimu ujao.


Henry ameiambia Salehjembe kwamba kikubwa anachovutiwa nacho Mwadui ni kwenda kucheza na wachezaji wazoefu na wakongwe ambao wapo kwenye kikosi hicho.


“Bado sijajua kama nitaendelea na Mtibwa ama vipi, kwa sababu bado nawasikilizia lakini hata timu nyingine pia nipo tayari kuzichezea, timu kama Mwadui ipo poa, katika hizi zilizopanda inaonekana kama iko poa kwenye uongozi na sehemu nyingine, ndiyo maana wamefika hapa.


“Halafu kitu kingine ina wachezaji wazoefu wa ligi ambao wengi nafahamiana nao, kwa hiyo nikicheza sehemu kama hiyo haitakuwa taabu sana kucheza mpira mzuri kwa kuwa wengi mno mnajuana na mnakuwa na morali ya aina moja katika mapambano,” alisema Henry.


Mwadui iliyo chini ya kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, imepanda kushiriki ligi kuu ikiwa na nyota wengi waliowahi kutamba huko nyuma lakini imeongeza pia wengine.


Baadhi ya wachezaji wao wazoefu ni Shaban Kado, Athuman Idd ‘Chuji’, Uhuru Selemani, David Luhende, Nizar na Razak Khalfan, Jabir Aziz na Rashid Mandawa.



0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video