Timu ya taifa ya wanawake ya England imefuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya kuwafunga wenyeji wa michuano hiyo timu ya Canada kwa goli 2-1 kwenye mchezo wa robo fainali uliopigwa usiku wa kuamkia leo.

Christine Sinclair alifunga goli pekee la kufutia machozi kwa upande wa wenyeji Canada akitumia makosa ya Karen Bardsley.
Hiyo ni mara ya kwanza kwa England kufika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo kwenye historia ya soka la wanawake nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment