Brazil imetupwa nje ya michuano ya michuano ya Copa America kwa mikwaju ya penati kufuatia kwenda sare ya kufungana goli 1-1 dhidi ya Paraguay kwenye dakika 90 za mchezo na kuufanya mchezo huo kuamuriwa kwa matuta ndipo Brazil walipotupwa nje ya mashindano kwa penati 4-3 kwenye mchezo wa robo fainali uliopigwa kwenye dimba la Ester Roa Rebolledo huko Chile.
Brazil ndio walikuwa wa kwanza kupata goli kwenye dakika za kawaida (90’) kupitia kwa Robinho aliyeifungia timu yake dakika ya 15 kipindi cha kwanza akiunganisha krosi maridadi aliyogongewa na beki wa pembeni wa FC Barcelona Dani Alves na kuipa timu yake matumaini ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya mataifa huko bara la America ya Kusini.



0 comments:
Post a Comment