Tuesday, June 9, 2015

Na Ramadhani ngoda.
Wagonga nyundo wa jiji la London, klabu ya West Ham United wamethibitisha Slaven Bilic kama kocha mkuu wa klabu hiyo baada ya makubaliano ya kusaini mkataba wa maka mitatu.
Mcroatia huyo ametwaa kibarua hicho kwa kumpiga chini Marcelo Bielsa aliyekuwa akiwania naye nafasi hiyo iliyoachwa na kocha aliyetimka klabuni hapo Sam Aladyce ‘Big Sam’


Bilic hakusita kuonesha furaha yake kurejea katika klabu aliyoichezea kwa miezi 18 tu mwaka 1996 na 1997.

“Nimefurahi kurudi West Ham United. Naikumbuka West Ham kama klabu ya kipekee sana. Nawapenda vijana wa klabu hii ya kipekee,” alisema Bilic.

“Kigezo change kikuu ninapochagua timu huwa nimalengo ya timu. Malengo na ari ya West Ham ipo katika kuwa klabu kubwa. Hiyo ni moja ya sababu kubwa iliyofanya nione kweli wananihitaji,” alisitiza Mcroatia huyo.

West Ham waliomaliza nafasi ya 12 katika msimu wa ligi uliomalizika wakivuna point 47, sawa na Everton na moja nyuma ya Crystal Palace waliomaliza wa 10, wapo katika harakati za kujenga kikosi kwa kuongeza baadhi ya wachezaji akiwemo kiungo Pedro Biang wa Sampdoria.


Licha ya kuongeza wanandinga wapya katika klabu hiyo, bado Bilic atakuiwa na kibarua cha kubakisha wachezaji waliotia nia kutimka Upton Park akiwemo mshambuliaji Carlton Cole.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video