Monday, June 8, 2015

MAKAMU bingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wanaanza mawindo ya ligi kuu na kombe la Kagame Juni 15 mwaka huu.
Afisa mtendaji mkuu wa Azam, Saady Kawemba amesema wachezaji wote wanatakiwa kuripoti kambini siku hiyo isipokuwa wale waliopo timu ya taifa.

“Tuliwapa wachezaji likizo ya mwezi mmoja, wanarejea kambini tarehe 15 isipokuwa wale waliopo timu ya taifa, makocha wote watawasili Juni 12 na kuanza maandalizi ya ligi kuu Tanzania bara na kombe la Kagame”. Amesema Kawemba na kusisitiza: “Kocha mkuu Stewart Hall yupo na anaendelea na kazi yake, anafanya kazi kuhakikisha mambo yote yanakwenda anavyotaka. Kuhusu usajili wa wachezaji anamsubiri mwenzake George Nsimbe (kocha msaidizi) ili wafanye kazi yao”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video