Monday, May 18, 2015

SIMBA inaendelea na usajili wa kimataifa lakini imepanga kuzunguka na kufanya utafiti kwa nchi tano hapa Afrika huku lengo likiwa ni kumtafuta straika mmoja tu atakayekuja kuziba pengo la Mganda, Dan Sserunkuma.
Simba imepanga kufanya usajili huo kwa kuwa tayari inaye straika mwingine atakayejiunga na timu hiyo msimu ujao, Mkenya, Paul Kiongera, anayetokea KCB ya Kenya alikokuwa akicheza kwa mkopo na kuimarisha kiwango chake baada ya kukaa nje kwa muda mrefu akiuguza majeraha aliyokuwa nayo baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, amesema nchi walizopanga kwenda kuangalia mchezaji wa nafasi hiyo ni pamoja na Burundi, Kenya, Senegal, Ghana na Uganda.

“Tunaamini tunaweza kupata straika mzuri mwenye uwezo wa juu katika nchi tano ambazo tuna imani nazo katika nafasi hiyo, tunaangalia katika nchi za Burundi, Kenya, Senegal, Ghana na Uganda. 

"Lengo ni straika mmoja, tukimaliza hapo tutakuwa na wachezaji wageni wanne na hiyo nafasi moja tutaangalia kama kutakuwa na usajili wa nafasi yoyote ya lazima,” alisema Hans Poppe.


Simba imeamua kuachana na Waganda wawili, Simon Sserunkuma na Dan Sserunkuma na sasa imebaki na Emmanuel Okwi, Juuko Murshid na Mkenya, Kiongera anayerejea.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video