Thursday, May 21, 2015


WACHEZAJI wa Yanga, Mbrazil Andrey Coutinho na Mliberia, Kpah Sherman, wamewekwa sokoni ili kuwapisha wachezaji wengine wa kigeni katika kikosi cha mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ipo katika mikakati ya kusajili wachezaji wa kiwango cha kimataifa ili waweze kufanya kweli kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani.
Akifanya mahojiano na gazeti la BINGWA jana, Katibu Mkuu Yanga, Jonas Tiboroha amesema kuwa wamedhamiria kufanya kweli kwenye usajili wao kuelekea msimu ujao, hivyo moja ya vigezo ambavyo uongozi wa timu hiyo unavizingatia ni pamoja na kusajili wachezaji watakaoendana na hadhi ya klabu hiyo.
“Tumedhamiria kufanya usajili wa nguvu msimu ujao, moja ya mikakati yetu ni kuhakikisha tunapata wachezaji wapya wa kigeni ambao watakuwa na uwezo mkubwa wa kuipa heshima Yanga na sio kusajili ovyo tena,” alisema Tiboroha.
Alisema kutokana na hilo, wameamua kuwaweka sokoni kiungo mshambuliaji, Coutinho na mshambuliaji, Sherman tayari kuwapisha wengine kuziba nafasi zao baada ya klabu yao kutoridhishwa na uwezo wa wawili hao.

Chanzo:Bingwa

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video