Man United sasa waitaka saini ya Sterling
KATIKA hali ya kushitukiza, Manchester United wametuma maombi Liverpool ya kujaribu kumsajili Raheem Sterling.
Hakuna mchezaji yeyote aliyejiunga moja kwa moja kutoka timu moja kwenda nyingine kati ya wapinzani hawa wakubwa wa soka la England (Liverpool na Man United) tangu Phil Chrinall alipotoka Old Trafford na kutua Anfield mwaka 1964, lakini sasa United wanaitaka saini ya Sterling.
Liverpool wamewaambia United kwamba hawana nia ya kufanya biashara ya Sterling ambaye alikataa ofa ya mkataba mpya na amemwambia Brendan Rodges kwamba anahitaji kuondoka majira ya kiangazi mwaka huu.
Sterling amebakiza miaka miwili katika mkataba wake wa sasa na Liverpool wameweka wazi kwamba hawataki kumuuza majira ya kiangazi.
Chelsea, Arsenal na Manchester City zinahusishwa kuiwinda saini ya nyota huyo wa kimataifa wa England, lakini United wameingia kwa nguvu kubwa.
0 comments:
Post a Comment