Ngassa amejiunga na Free State Stars
SIKU moja tu baada ya mama mzazi wa mshambuliaji wa
kimataifa wa Tanzania aliyesajiliwa na Free State Stars ya Afrika kusini,
Mrisho Ngassa, kumtaja mwanachama wa Yanga, Shamte Mkumba kuwa ndiye aliyehusika kumzuia
mwanae kujiunga na El Merreikh ya Sudan wakati huo, mdau huyo wa soka ametoa
ufafanuzi wake.
Mkumba amesema yeye alimzuia Ngassa kujiunga El Merreikh kwa
sababu za maslahi yake mwenyewe.
“Mrisho Khalfan Ngassa riziki yake kwenda El Merreick
ilikuwa haijatimia, sahizi umeona riziki imetimia ameenda Afrika kusini. Wananchi wajue kwamba Mrisho hakutaka
kuuzwa kama gunia na ukimuuliza yeye hilo suala anajua”. Amesema Mkumba na
kusisitiza: “Ngassa alitaka auzwe na apate faida, alikuwa hataki kuuzwa ili
wengine wapate faida, kumbuka lile dili la El Merreikh, klabu mbili zilitaka
kugawana dola laki moja na nusu za usajili, dola elfu 75 wachukue Simba dola 75
wachukue Azam. kitu kile kilimuuma sana Ngassa na hakutaka kwenda El Merreikh
kwa kuwafaidisha watu wengine.
“Mrisho na Yanga wakakaa meza moja na kumpatia hela zaidi ya
ile aliyotaka kwenda El Merreikh, watu wagundue hilo. Mrisho alibaki kwa faida,
hakubaki Yanga kwa hasara, alipata hela zaidi ya ile ya El Merreikh, alipata mshahara
mzuri na posho nzuri Yanga”.
0 comments:
Post a Comment