Friday, May 15, 2015


HASSAN Ramadhan Kessy wa Simba imetajwa na makocha wengi wa ligi kuu, wasiokuwa wa ligi kuu na wachambuzi wa soka kuwa ndiye mlinzi bora zaidi wa kulia katika msimu wa ligi kuu 2014/2015 uliomalizika mei 9 mwaka huu.

Kessy amekuwa msaada mkubwa kwa Simba na mafanikio waliyoyapata ya kushika nafasi ya tatu yeye pia ni chachu kubwa.

Uwezo wake wa kupandisha mashambulizi na kugeuka kuwa winga aliyekamilika kila anapovuka mstari wa kati, ufundi wa kupiga pasi za mwisho, kupiga krosi na kurudi kwa haraka kukaba pale timu inapopoteza umiliki wa mpira ni miongoni mwa sababu zinazomfanya Kessy atajwe kuwa mlinzi bora na wa kisasa wa kulia kwa sasa nchini.

Licha ya kutajwa na makocha wengi kuwa ndiye bora, unaweza kudhani Kessy atakuwa na maneno mengi ya kukubali sifa hizo, lakini haiko hivyo.

Kessy ameiambia MPENJA BLOG neno moja kubwa baada ya kupata mafanikio Simba akisema: “Daah! Kiukweli Mungu ndiye anayejua kaka! Naendelea kumtumainia na kujifunza kila siku”.


Kuhusu kutoitwa timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’ Kessy amesema: “Mpira tunacheza, kila mtu ana malengo ya kufika mbali, lakini ndio hivyo siitwi timu ya Taifa, lakini wakati wangu unakaribia kabisa”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video