Mandawa (kulia) akijaribu kumpiga chenga mlinzi wa Yanga, Rajabu Zahir walipochuana uwanja wa Taifa msimu uliopita. Kagera Sugar ilifungwa 2-1.
MTANDAO huu jana uliripoti taarifa za Straika hatari wa
Kagera Sugar, Rashid Mandawa kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia timu ya
Mwadui fc iliyopanda kucheza ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2015/2016.
Leo hii tunakuletea kauli aliyosema Mandawa baada ya
kuanguka kandarasi hiyo kuwatumikia matajiri hao wa Madini wanaotarajiwa
kusumbua katika soka la Bongo.
“Kikubwa ni kumuomba mwenyezi Mungu, yeye ndiye mpangaji wa
kila kitu, yeye ndiye alinitoa kutoka chini na kuwa moja ya wafungaji bora. Namuomba
Mungu anizidishie zaidi ya hapa ili msimu ujao niweze kuchukua kiatu cha
ufungaji bora”, Amesema Mandawa na kusisitiza: “Mimi msimamo wangu kama
tulivyosaini mkataba , nitasaini mkataba mwingine pale utakapoisha, siwezi
kusaini mkataba wakati nina mkataba mwingine, kwanza nitakuwa najihatarisha
mimi mwenyewe na uchezaji wangu, unaweza kufungiwa miaka miwili na mimi kazi
yangu mpira.
Mandawa alifanikiwa kufunga magoli 10 akiwa na Kagera Sugar
msimu wa 2014/2015 uliomalizika mei 9 mwaka huu.
Simon Msuva wa Yanga ndiye aliyeibuka mfungaji bora wa ligi kuu baada ya kutikisa nyavu mara 14.
0 comments:
Post a Comment