Kamati ya Usajili ya Simba,
imefanya kweli kwa kuwabakiza wachezaji wake wawili, Said Ndemla na Hassan
Isihaka.
Isihaka ambaye ni nahodha wa
Simba, ilielezwa alikataa kusajili kwa madai nataka dau nono zaidi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,
Zacharia hans Poppe amesema tayari wamemalizana na wachezaji hao kwa
kuwaongezea mikataba ya miaka mitatu kila mmoja.
“Wote wawili, kila mmoja tumemuongezea mkataba wa miaka mitatu,” alisema Hans
Poppe.
“Tunaendelea kufanya
mazungumzo na wengine ambao tunahitaji wabaki. Kidogo tunafanya mambo yetu
hatua kwa hatua.”
Simba tayari imeanza kufanya
usajili wa kuboresha safu yake ya kiungo lakini walichopanga kwanza ni
kuwabakiza wachezaji wanaowataka.
Hans Poppe ndiye mwenyekiti
wa kamati hiyo na makamu wake ni Kassim Mohammed Dewji.
0 comments:
Post a Comment