Kipanga (kulia) alikuwa kwenye rada za Simba mwaka jana
MSHAMBULIAJI nyota wa Mbeya City Fc, Saad Kipanga amesema bado anataka kuwa sehemu ya kikosi cha timu hii msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Akizungumza mapema leo Kipanga aliyemalizia msimu akicheza kwa mkopo kwenye timu ya Polisi Tabora iliyokuwa inashiriki ligi daraja la kwanza Taifa, alisema kuwa anafurahi kurejea tena kwa kiwango chake baada ya kufanikiwa kucheza vizuri kwenye kikosi cha Polisi.
“Nimemaliza msimu nikiwa Polisi kwa mkopo, nashukuru nimecheza michezo 7 na kufunga goli 6, hili ni jambo zuri kwangu kwa sababu limenifanya kuamini kuwa kiwango changu kimeimarika na ninaweza tena kucheza vizuri nikiwa kwenye kikosi cha City, kuna timu nyingi zinataka huduma yangu lakini nataka kubaki hapa kwa sababu nina amini nitafanikiwa zaidi” alisema.
0 comments:
Post a Comment