Friday, May 22, 2015

 

WAKATI Azam fc wakidai idadi ya wachezaji wa kigeni ligi kuu soka Tanzania bara iongezwe kutoka idadi ya sasa ya watano, kocha wa Mbeya City fc, Juma Mwambusi amepinga mtazamo huo.
Hoja ya Azam kutaka idadi iongezeke ni kupata wachezaji wengi wa kigeni watakaowasaidia katika michuano ya kimataifa pamoja na kuwapa changamoto wachezaji wazawa ndani ya timu hiyo.
Makamu bingwa hao wa ligi kuu msimu wa 2014/2015 wanadai wamejifunza kwa TP Mazembe na El Merreikh ambao wamesheheni wanasoka wengi kutoka nje ya nchi zao.
Azam wakitoa hoja hizo, Mwambusi amesema haoni haja ya kuongeza wachezaji wa kigeni bali vipaji vya ndani viangaliwe zaidi.
“Siungi mkono kuongeza idadi ya wachezaji wa kigeni katika soka letu la Tanzania kwasababu sisi tuna wachezaji wengi wenye vipaji. Muhimu ni wachezaji wetu kujitambua kwanza, halafu viongozi wa klabu zetu wanawachukuliaje wachezaji wetu?” Amesema Mwambusi na koungeza: “Saa nyingine watu wanataka kusajili kwa fasheni, vilabu vikubwa vinashindana kusajili wachezaji wa nje, tusichukue wachezaji kwasababu tu tunataka kushindana na fulani, tuwachukue wachezaji wa nje kwasababu wana kiwango cha juu ili waje kuleta changamoto hapa kwetu”.
“Kwa idadi iliyopo inatosha kwasababu tumeshaona hata hao watano kuna wengine wanakaa nje kwa kushindwa na wazawa. Mimi nasema wachezaji wetu wanatakiwa kujitambua tu ili wajue kuwa mpira ni kazi, wajitoe na kucheza kwa juhudi zote uwanjani ili kuweza kuendeleza soka letu”.
“Wanaweza kuja hata wachezaji 11 wa kigeni, sijui kama itatusaidia, kikubwa tuangalie tulipojikwaa, tusiangalie tulipoangukia. Viongozi wanaweza kusema vijana wetu hawajitambui, sawa!, watajitambuaje? Kila mtu kwa nafasi yake katika mpira afanye kazi kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na kwa umakini mkubwa, viongozi wanaotawala soka katika nchi yetu wana nia kweli ya kuendeleza soka letu?. Tunaweza tukakubali kuleta wachezaji wengi, lakini tusipopita kwenye mfumo sahihi hatuwezi kufika kokote”.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video