KIUNGO mshambuliaji wa Mbeya City fc, Deus Kaseke amekanusha
taarifa zinazoendelea kusambaa kwamba amesaini kuichezea Yanga msimu ujao wa
ligi kuu soka Tanzania bara.
Hata hivyo Kaseke amesema yupo tayari kuondoka Mbeya City
kwenda klabu yoyote itakayompa maslahi mazuri, lakini kwasasa yupo katika
mazungumzo ya awali na klabu za Simba na Yanga.
“Mimi sijasaini klabu yoyote, namaliza mkataba Mbeya city
mwezi wa sita, bado sijafanya mazungumzo na viongozi wa klabu yangu. Simba na Yanga
wananitafuta, mazungumzo yanaendelea, mpira kazi yangu, naangalia maslahi yangu
binafsi”. Amesema Kaseke na kusisitiza: “Mimi niko tayari kuondoka Mbeya City
timu yoyote ikinipa maslahi mazuri, lakini jua sijasaini Yanga. Simba tuna
mazungumzo ya awali tu, lakini hatujaafikiana, kuna wakala wangu anayenisimamia”
0 comments:
Post a Comment