Sunday, May 31, 2015

Timu ya Cairo kutoka Misri imefanikiwa kutetea taji lake la ubingwa wa mpira wa kikapu wa michuano ya majiji ya Afika Mashariki na Kati (East & Central Africa Inter-Cities Championship) baada ya kuifunga timu ya Qardho ya Somalia kwenye mchezo wa fainali uliopigwa leo jioni kwenye uwanja wa ndani wa Taifa.
Mchezo huo ulioshuhudiwa na mamia ya wakazi wa Dar es Salaam wakiongozwa na Balozi wa Misri nchini Tanzania pamoja na mama wa nyota wa mchezo huo Hasheem Thabiti. Pambano hilo lilikuwa na upinzani mkali kutokana na timu zote mbili kuonesha viwango vya juu hali iliyoufanya mchezo huo kuwa mkali na wakuvutia zaidi.

Cairo ilifanikiwa kutwaa ubingwa huo kwa kuifunga timu ya Qardho kwa jumla ya vikapu 79 kwa 59 na kutetea taji hilo ambalo walilitwaa pia mwaka uliopita. Mechi hiyo ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa mchezo wa kikapu kutokana na timu hizo kutoa vipigo vikali kwa timu za Tanzania hivyo ilikuwa ikisubiriwa kuona nani ataibuka mbabe na kutwaa ubingwa huo kati ya timu hizo mbili.
Kwa upande wa wanawake, timu ya Nairobi City imenyakua ubingwa baada ya kuilaza timu ya Kampala City wakati timu za Tanzania zimeendelea kuwa wasindikizaji kwenye michuano hiyo mikubwa ya kikapu kwa ngazi ya majiji ya Afrika Mashariki na Kati.



Mashindano hayo yaliyoshirikisha jumla ya timu10 kutoka kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kati. Nchi hizo zilikuwa ni pamoja na Tanzania ambao walikuwa wenyeji, Kenya, Uganda, Somalia pamoja na Misri yalianza Mei 27 na leo Mei 31 ndio ilikuwa siku ya kufunga pazia la michuano hiyo ambapo inatarajiwa kufanyika mwaka ujao kwa mara nyingine.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video