AZAM FC wanasuasua kumtangaza rasmi Muingereza Stewart John
Hall kuchua nafasi ya kocha aliyeachishwa kazi, Mcameroon, Joseph Marius Omog.
Stewart na Azam kimsingi wamemalizana, kilichobaki ni
kutangazwa rasmi pamoja na wasaidizi wake ambao tayari wameshasaini mikataba mipya,
George ‘Best’ Nsimbe (msaidizi namba moja) na Dennis Kitambi (msaidizi namba
mbili).
Kinachochelewesha kutangazwa kwa Stewart ni kumsubiri
amalizane na waajiri wake, Symbion Power ambapo anafanya kazi kama mkurugenzi
wa kituo cha soka cha vijana kinachojengwa na kampuni hiyo jijini Dar es salaam.
Stewart aliwaandikia Symbion barua ya kuomba kuacha kazi ‘Notice
letter’ ya siku 30 na akimalizana nao ataanza kazi rasmi Azam fc juni 15 mwaka
huu.
Katibu mkuu wa Azam fc, Nassor Idrissa ‘Father’ amesema siku
si nyingi watamtangaza kocha mpya ambaye hajataka kumtaja, lakini hakuna shaka
yoyote ni Stewart kwa asilimia 100.
“Suala la kocha litamalizika baada ya siku mbili zijazo,
tunataka kutangaza kitu kilichokamilika, kutangaza kuwa tumeingia kandarasi na
kocha fulani nafikiri ni siku mbili, tatu tu zijazo”. Amesema ‘Father’ na
kusisitiza: “Suala la mchezaji au kocha sio la kificho, lakini kama unavyojua
masuala yao ni ya kimkataba na sheria, sisi kama klabu hatuwezi kupaza sauti
zetu moja kwa moja wakati mambo ya kimkataba hayajakaa sawa, muda mchache ujao
tutaweka kila kitu hadharani”
“Walimu ambao tumekaa nao kwenye meza ni pamoja na mwalimu
Stewart Hall, tutawatangazia kama ni yeye anachukua nafasi au mwingine”.
0 comments:
Post a Comment