Monday, April 27, 2015


UONGOZI wa Yanga umewakaribisha wananchi wote kujitokeza leo uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kusherekea ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania.

Yanga inakabiliana na Polisi Morogoro katika mechi ya ligi kuu itakayoamua ubingwa kwasababu wanahitaji pointi tatu tu kutawazwa mabingwa wapya.

Mpaka sasa Yanga wanaongoza katika msimamo wa ligi kuu kwa pointi 52 na kama watashinda leo watafikisha pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote.

Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro ameuambia mtandao huu kuwa uongozi umeandaa ‘staili’ ya aina yake kushangilia ubingwa leo.


“Kama una wasiwasi kuwa Yanga hawawezi kuwa mabingwa leo basi una matatizo, kama kawaida yetu leo tunabeba kombe kwa kumpiga mtu (Polisi Moro) goli nyingi”. Amesema Muro na kuongeza: “Hakuna wa kutuzuia, wananchi waje kwa wingi kushangilia ubingwa wetu wa mapema”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video