Tuesday, April 28, 2015

Mshambuliaji wa Man United Robin van Persie, ameonesha dalili zote kwa kocha wake Louis van Gaal kuwa bado anahitaji kubaki klabuni hapo baada ya msimu huu kumalizika.
Van Persie ambaye msimu huu ameitumikia klabu hiyo mara chache kutokana na kuandamwa na majeruhi ya mara kwa mara, amecheza mechi 25 huku akifunga magoli 10 tu katika michuano yote.
Van Persie anajua fika kuwa siku zake za kubaki klabuni hapo zinahesabika huku Van Gaal ikisemekana yupo mbioni kuingia sokoni kutafuta mshambuliji mwingine ambaye atakuwa akisaidia na Rooney ambaye ndiyo nahodha wa timu hiyo.
Lakini hata hivyo Van Persie mwenye ambaye atakuwa anatimiza miaka 32 kabla ya msimu ujao kuanza anasemekana kuyafurahia maisha ya klabuni hapo na yupo tayari kuendelea kuitumikia klabu hiyo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video