Tuesday, April 28, 2015


BODI ya ligi kuu soka Tanzania bara (TPLB) kupitia kwa mwenyekiti wakati Ahmed Yahya bado haijapanga siku rasmi ya kuwakabidhi Yanga ubingwa wao na zawadi nyingine.
Yahya amesema siku ya kuwakabidhi ubingwa ni baada ya ligi kuu kumalizika na hawezi kuwakabidhi wakati ligi bado haijamalizika.
“Siku (ya kukabidhi ubingwa) haijapangwa bado kwasababu ligi haijamalizika, ligi ikimalizika tutapanga siku ya kutoa zawadi na kuwakabidhi ubingwa wao rasmi, lakini wana haki ya kushangilia. Nitumie nafasi hii kuwapongeza Yanga kwa kuibuka mabingwa wa Tanzania bara”.
“Hatuwezi kuwakabidhi ubingwa mapema kwasababu tunafuata sheria na kanuni zetu, tutawakabidhi baada ya kumalizika kwa mashindano, hatuwezi kuwakabidhi hapa katikati, ni mabingwa kwa matokeo, lakini ligi bado haijaisha, ligi inamalizika tarehe 9 mwezi wa tano, hapo tutakuwa na nafasi kuwakabidhi ubingwa na zawadi nyingine zikafuata baadaye kidogo”.
Mchana wa leo shirikisho la soka Tanzania bara, TFF, kupitia kwa afisa habari wake, Baraka Kizuguto lilituma taarifa kwa vyombo vya habari likieleza kuwa Yanga watakabidhiwa ubingwa aprili 6 mwaka huu kwenye mechi ya ligi kuu baina ya Azam fc na Yanga.
Lakini kauli ya mwenyekiti wa bodi inaonesha kutofautiana na TFF.
Taarifa iliyotumwa mchana kwa vyombo vya habari na Baraga Kiziguto hii hapa:
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF, Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa klabu ya Young Africans, Yusuf Manji kufuatia timu yake kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2014/2015.


Katika salamu zake za pongezi, Malinzi amesema kutwaa Ubingwa wa VPL ni jambo muhimu na sasa wanapaswa kuanza maaandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa barani Afrika mwakani.


Klabu ya Young Africans imetwaa Ubingwa wa Ligi Kuu nchini kwa mara ya 25 (ishirini na tano) jana, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya timu ya Polisi Morogoro katika uwanja wa Taifa huku ikiwa na michezo miwili mikononi kabla ya ligi kumalizika.


Waziri wa Habari, Vijana Utamuduni na Michezo, Dr. Fennela Mkangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kukabidhi Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Mei 6, 2015 katika mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Young Africans.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video