Wednesday, April 29, 2015


Rais Malinzi

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF, Jamal Malinzi aprili 27 mwaka huu amefungua kozi ya walimu wakufunzi wa mpira wa miguu nchini inayofanyika katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam ikitarajiwa kumalizika mei 2 mwaka huu.

 Malinzi alisema kozi hiyo ni muhimu kwa mustakabali wa soka la Tanzania, walimu wakufunzi watasaidia kuwafundisha walimu wengine wa mpira, ili kuweza kufundisha mpira kwa watoto wadogo ambao ndio hazina ya baadae.

 Malengo ya TFF ni kuhakikisha timu ya vijana ya U17 inafuzu kwa fainali za Mataifa Afrika 2017 nchini Madagscar, na baadaye kuwa na kikosi bora wakati tunapotarajia kuwa wenyeji wa fainali za U17 Afrika mwaka 2019. 

Ili kufanikisha malengo hayo, TFF imeeleza  program mbili za kuwaandaa vijana wenye umri chini ya miaka 13, 15 kwa kuwaweka kambini na kucheza michezo ya kirafiki mikoani na kufanya ziara katika nchi za Malawi, Zambia, Zimbabwe, Bostwana na Afrika Kusini. Pia ina malengo ya kuanzisha mashindano ya vijana chini ya miaka 13 yatakayofanyika Alliance Mwanza kwa lengo la  kuibua vipaji.

Ukipima malengo ya TFF ni mazuri wala hayana shaka, lakini kufanikiwa ni ndoto kwasababu kuna mambo ya msingi ambayo hayajafanyiwa kazi.

Mtandao huu unatambua juhudi za Rais Malinzi, lakini unakataa mpango wake wa soka la vijana na kumshauri mambo saba ambayo anatakiwa kuyafanyia kazi kabla ya kuanzisha mashindano;

 Iwekwe wazi kuwa huwezi kuanzisha mashindano ya vijana chini ya miaka 13 kwa lengo la kutengeneza timu moja au mbili ili vijana waandaliwe kucheza mashindnao ya Afrika. Hili sio suluhisho la maendeleo ya mpira wa nchi.

Mosi; Malinzi atengeneze falsafa ya mpira wa nchi ya Tanzania, ikishapatikana falsafa itakuwa ni rahisi kwa kijana aliyetoka Zanzibar, Pemba, Manyara, Lindi kufundishwa mpira wa aina moja kwasababu tayari  kuna falsafa ya nchi ambayo pia itaingia moja kwa moja kwenye timu za ligi kuu. Kwa mfano ukiangalia ligi ya Ujerumani, Bundesliga, ukiangailia ligi ya Hispania, La Liga au Uholanzi, inavyocheza timu ya taifa ukienda kwenye klabu utaona wanacheza vilevile, mathalani, wanavyocheza Barcelona, Real Madrid, Valencia utaona wanacheza hivyo hivyo kwenye timu ya Taifa ya Hispania.

Ukienda Ujerumani ‘Staili’ ya uchezaji wa klabu inaendana na timu ya taifa. Hii ndio maana ya falsafa, kama taifa mnaamua kwamba hii ndio staili yetu ya uchezaji, kufundisha wachezaji na hapo ndipo unapata urahisi wa kufundisha mpira. Kabla ya kukimbilia kwenye mashindano kwanza ni kukaa chini na wataalamu ili kutengeneza falsafa ya mpira wa Tanzania.

Pili; Malinzi atengeneza mfumo sahihi wa kutambua na kuendeleza vipaji katika ngazi zote ikiwemo umri chini ya miaka 13. Yeye anasema yatafanyika mashindano pale Alliance Mwanza, lakini haiwezekani watu wakaja kucheza tu, lazima uwepo mfumo thabiti wa kung’amua vipaji kote nchini kupitia vyama vya wilaya na vyama vya mikoa. Kuwepo mfumo unaofanana wa kutambua vipaji kila kona ya nchi na kuviendeleza.

Mashindano ya vijana yatafanyika, lakini kama hakuna mfumo mzuri wa kimashindano wa kubaini vipaji na mfumo wa kuviendeleza vipaji hivyo, lengo halitafanikiwa. Wachezaji ambao wamekamilika kiushindani hawatapatikana. Itengenezwe falsafa baada ya hapo utengenezwe mfumo wa kuviendeleza vipaji na itakuwa rahisi kupata timu bora.

Tatu; Uandaliwe mfumo mzuri wa kupata viongozi madhubuti, viongozi wenye uwezo. Haiwezekani Malinzi akawa na malengo yake peke yake kwamba tunataka kucheza fainali za Afrika chini ya umri wa miaka 17 wakati kwenye vyama vya mikoa au wilaya kuna watu hawaelewi wala kuona kile unachowaza yeye.

Ni lazima kutengeneza mfumo mzuri wa kitaifa wa kuwa na watu sahihi kuanzia ngazi zote, viongozi ambao wana uwezo wa kutekeleza mawazo yake kama kiongozi wa juu. Sawasawa na wewe ni mmiliki wa kampuni, una malengo ya kufikia malengo fulani kumbe wafanyakazi wako wote ni ‘vimeo’. Unafikiaje malengo wakati huna wafanyakazi wenye mawazo na matazamo kama wakwako?. Tuna tatizo la kiuongozi katika ngazi ya vyama na kwenye klabu pia. Lakini kama nilivyosema mwanzo ukiwa na falsafa itakuongoza kujua ni aina gani ya viongozi na wachezaji uwe nao.

Kitu cha nne;  kabla ya mashindano kufanyika, Malinzi atengeneze mfumo wa kimashindano wa kitaifa kwa ngazi zote za kitaifa. Mfumo ule ule wa mashindano ya watoto ufanane kote nchini, ukienda Mbeya, Mwanza, Lindi, Pemba uone mfumo mmoja wa mashindano ili ukipata wachezaji wafanane kiuchezaji.

Tano, Malinzi  afundishe na kuzalisha makocha wa kutosha, angalau kuwepo uwiano wa kocha mmoja kufundisha vijana 30, hapa inategemeana na bajeti yake, mfano kama anataka awe na vijana elfu 10 wanaocheza mpira, inatakiwa awe na makocha wengi, huwezi kuwa na idadi hiyo ya vijana halafu ukawa na makocha watatu, lazima ujiulize kuna makocha wangapi nchi hii waliojikita kwenye ufundishaji wa soka la vijana? Itakuwa ni ndoto za mchana kutaka kutengeneza mashindano wakati miondombinu ya kupata makocha hakuna.

Ukizalisha makocha wengi watakuwa na  nafasi ya kufundisha vijana wengi unaotaka kuwaandaa. Uanzishwe mpango madhubuti wa kuzalisha makocha wengi. Uwiano wa sasa unakuta kuna vijana elfu tatu halafu kocha mmoja, inawezekana kocha mmoja kufundisha vijana elfu tatu? Haiwezekani!. Kama nilivyogusia hapo juu , kama unataka kuwa na idadi kubwa ya vijana pia unatakiwa kuwa na wataalamu wengi wa kung’amua vipaji na kuviendeleza, usipokuwa na wataalamu utaishia kutengeneza kundi la wachezaji wa zamani na kuwagawa kwa maeneo wakati utaalamu wenyewe wa kubaini wachezaji hawana.

Sita; Malinzi aboreshe miondombinu ya mpira na utawala kwenye ngazi zote. Nilizingumzia kidogo mwanzoni kuhusu viongozi, nasisitiza tena, uboreshe miondombinu ya kiuongozi kwenye ngazi ya taifa, mikoa na wilaya. Lazima kuwepo na mabadiliko chanya ya kuendana na usasa ili uwepo uhalisia wa kufikia malengo tuliyojiwekea ya kucheza michuano ya Afrika. Hata kama tutakuwa wenyeji lazima tushindane, lazima tutafute wataalamu na kuacha kukwepa njia sahihi.

Jambo la saba ni kufanya utafiti na kubaini mbinu sahihi za kufundishia, kuna mabadiliko makubwa sana ya kiufundishaji, kabla ya kuanzisha mashindano ya kupata vijana, lazima tukae chini kufanya utafiti mzuri kupata njia sahihi za kufundishia mpira. Lazima utengenezwe mfumo mzuri wa kisayansi wa kuweza kufundisha soka. Pia miundombinu bora ya kitabibu kwa ajili ya kuwapatia wachezaji tiba nzuri, waweze kupewa ushauri mzuri vya vyakula, sio kukimbia tu na kucheza mpira.

Hitimisho ni kwamba; kabla ya mashindano hayo kuanza, Jamal Malinzi anatakiwa kuyapa kipaumbele mambo haya saba ili kutimiza malengo ya kuona Tanzania inacheza fainali za vijana za Afrika na kombe la Mataifa ya Afrika kwa timu ya wakubwa (Taifa Stars), bila kufanya hivyo ni kutwanga maji kwenye kinu.


Nawakakia jumatano njema, tukutena tena ijumaa panapo majaaliwa!! Ni halali yako kutoa maoni au mtazamo wako!

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video