Tuesday, April 28, 2015


UONGOZI wa Bodi ya ligi kuu Tanzania bara (TPLB) umewatahadharisha mabingwa wa ligi kuu msimu huu 2014/2015, Dar Young Africans kutojihusisha na upangaji wa matokeo katika mechi zao mbili zilizosalia.
Yanga watacheza na Azam fc uwanja wa Taifa aprili 6 mwaka huu na kumalizia ligi uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara dhidi ya wenyeji Ndanda fc mei 9 mwaka huu.
Mechi  ijayo haina faida wala athari yoyote kwa Yanga, lakini inaweza kuwaharibia zaidi Azam kama watafugwa kwasababu itakuwa inatoa mwanya kwa Simba kuiwania nafasi ya pili.
Lakini kwa vile Yanga ni maadui wa kimpira wa Simba na hawataki wapande ndege mwakani kwenye mashindano ya CAF, kuna maneno ya hapa na pale kwamba Wanajangwani wanaona bora kufungwa na Azam ili kuwatengenezea mazingira ya kuchukua nafasi ya pili lakini sio watani wao wa jadi Simba.
Machi 8 mwaka huu, Yanga ilifungwa goli 1-0 na Simba kwenye mechi ya ligi kuu na kipigo hicho kimetia doa ubingwa wao, hawafurahii kuchukua ubingwa huku wakiwa wamefungwa na Simba.
Mwenyekiti wa Bodi ya ligi kuu, Ahmed Yahya amewataka Yanga kucheza mpira kwa kufuata kanuni na sheria za mchezo katika mechi zao zilizosalia.

“Yanga wajijue kuwa bado wana jukumu katika ligi hii, mechi hazijamalizika, wacheze mpira, wanaweza kushangilia ubingwa halafu mwisho wakaanza mambo ya maajabu, wakatuharibia ligi yetu
“. Amesema Yahya na kuongeza: “ Nina maana kwamba wao wameshakuwa mabingwa, wanaweza kuona hawana majukumu tena katika ligi hii, wao waendelee kucheza mpira uwanjani na kujiepusha na mipango ya nje ya uwanja” Amesema Yahya.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video