Tuesday, March 3, 2015




Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,
Yanga SC hawajapoteza mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya mahasimu wao Simba SC kwa msimu wa tatu sasa, na mchezo ujao wa ‘ Dar es Salaam derby’ siku ya Jumapili ijayo utakuwa ni mchezo wa sita. Mara ya mwisho Simba kuishinda Yanga katika ligi kuu ni Mei 7, 2012 walipochomoza na ‘ ushindi mkubwa zaidi katika karne’ . Simba ilishinda mabao 5-0 msimu ambao walitwaa ubingwa wao wa mwisho katika ligi kuu.

Yanga imeifunga Simba mara moja tu katika michezo mitano iliyopita ya ligi kuu na wataingia kwa mara ya sita mfululizo ‘ wakiwa katika umbo la ushindi’ siku ya Jumapili ili kukamilisha msimu wa tatu pasipo kufungwa na mahasimu wao hao katika ligi kuu.  Msimu wa 2012/13 timu hizo ‘ watani wa jadi’ zilifungana bao 1-1 katika mchezo wa mzunguko wa kwanza, kisha Yanga ikaishinda Simba kwa mabao 2-0, Mei, 2013 na kutwaa ubingwa wao wa 24.

Msimu wa 2013/14 timu hizo zilitengeneza ‘ mchezo wa aina yake’, Oktoba, 2013. Yanga walimaliza dakika 45 za kwanza wakiwa katika kiwango cha juu huku wakiwa mbele kwa mabao 3-0, kufikia dakika ya mwisho ya mchezo huo Simba ‘ walikomboa’ magoli yote na kutengeneza sare ya 3-3. Katika mchezo wa marejeano siku ya mwisho ya msimu, April 24, 2014 Yanga walisawazishia kupitia kwa Saimon Msuva zikiwa zimesalia dakika chache mchezo kumalizika na kutengeneza sare ya kufunga bao 1-1.

Oktoba, 2014 timu hizo zilitengeneza sare ya nne mfululizo katika ligi kuu baada ya kumaliza dakika 90 bila kufungana. Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza msimu huu Yanga waliingia uwanjani wakiwa na matumaini makubwa ya kushinda lakini wakajikuta wakibanwa mbavu na Simba ambayo ilianza na wachezaji sita kutoka timu yao ya pili.

Patrick Phiri ndiye mwalimu wa mwisho wa Simba kuikabili Yanga katika ligi kuu. Phiri alitimuliwa klabuni hapo mara baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Kagera Sugar mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka jana. Nafasi ya Mzambia huyo kwa sasa ipo chini ya Mserbia, Goran Kopunovic. Goran hajawahi kushiriki katika mchezo wa ‘ Dar es Salaa Pacha’, baada ya kufanya kazi Rwanda na Vietnam, Goran atakutana na presha kubwa katika mchezo wa ‘ tatu kwa ukubwa barani Afrika’. Mchezo ambao mashabiki huzimia na wengine hupoteza maisha kwa bahati mbaya kutokana na presha.

Marcio Maximo ndiye mwalimu wa mwisho kuifundisha Yanga katika ligi kuu, mkufunzi huyo raia wa Brazil alitimuliwa kazi mara baada ya Yanga kufungwa na Simba mabao 2-0 Disemba, 2014 katika mchezo wa hisani wa ‘ Nani Mtani Jembe-2’. Lakini katika ligi kuu kocha huyo aliendeleza kutunza rekodi ya Yanga kutofungwa na Simba tangu waliporuhusu kipigo kikubwa cha mabao 5-0 miaka mitatu iliyopita. Maximo ndiye mwalimu aliyeiongoza Yanga katika suluhu ya 0-0 Oktoba mwaka jana.

Hans tayari anajua presha ya SIMBA NA YANGA kwa kuwa tayari alishawahi kuiongoza Yanga kusawazisha katika mchezo wa mwisho wa msimu uliopita. Ni kocha ambaye ameifanya Yanga kuwa na mchezo wa kushambulia na kufunga mabao. Kumbuka Yanga haifungwa na Simba katika ligi katika michezo mitano mfululizo huku wakishinda mara moja. KUELEKEA ‘ Dar es Salaam derby ‘ Jumapili hii niteendelea kukuletea rekodi zinazocheza kuhusu mahasimu hao. Kesho tutatazama ‘ Mbinu na ufundi wa makocha’


0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video