Wednesday, March 4, 2015


Na kosseyi deogaratius;

KIUNGO mpiganaji wa Chelsea Nemanja Matic aliadhibiwa kukosa mechi tatu kwa kosa la kutaka kulipiza kisasi kufuatia rafu mbaya aliyochezewa katika pambano lao dhidi ya Burnely.Hata hivyo alipunguziwa adhabu na kuwa mechi mbili kufuatia klabu yake kukata rufaa.Tayari amekosa pambano la fainali la Capital One ambapo Chelsea imeweza kutwaa taji hilo dhidi ya Spurs.Pia atakosa pambano gumu dhidi ya West Ham ambapo Chelsea inapigana kutanua pengo la pointi 8 dhidi ya Manchester city.
Kwangu mimi adhabu ya Matic ina faida kubwa mbili kwa Chelsea. Kwanza anapata muda mwingi wa kumpuzika kabla ya pambano gumu sana la marudiano dhidi ya PSG,lakini pia anahifadhi nguvu zake ambazo ni muhimu sana kwa timu yake katika kumalizia ligi
Faida nyingine ni kuwa adhabu yake inamfanya akose mechi,hii ina maana kuwa inamweka kando na uwezekano mkubwa wa kupata na majeraha.Ikumbukwe kuwa ligi ya wingereza ni ngumu sana katika mechi za kumalizia hasa kwa timu zinazopigania taji na zile zinazojiokoa na kushuka daraja.Kwa maana hiyo basi atakaporejea atakuwa na msaada mkubwa kwa timu yake kumalizia ligi.
Hakuna shaka matic ni mtu muhimu mno kwa Chelsea.Tazama pambano la chesea kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Newcastle Matic hakuwepo uwanjani.Pia kipigo cha mabao 5-3 kutoka kwa Spurs Matic hakuwepo uwanjani,hata ile sare ya 1-1 dhidi ya Burnely ilikuja mara baada ya  Matic kutolewa kwa kadi nyekundu.Hata pambano la fainali ya capital one japokuwa Chelsea ilifanikiwa kushinda lakini ilizidiwa mno na Spurs kwenye eneo la kiungo.Nacer Chadli,Nadeer Bentaleb na Lee Mason waliitawala Chelsea katika kiungo.

Haina ubishi Matic ni muhimili mkubwa kwa Chelsea.Uwepo wake uwanjani unaifanya Chelsea iwe na uwiano wa kushambulia na kuzuia.Timu nzima inacheza kwa uhuru.Eden Hazard,Willian na Fabrigas wanakuwa na jeuri ya kushambulia kwakuwa wanajua nyuma kuna mtu anaelinda timu.Safu ya ulinzi inakuwa na utulivu mkubwa kwasababu mbele yake kuna Matic.Kama ilivyo kwa Yaya Toure kwa Man city ndivyo ilivyo kwa Matic kwa Chelsea.Matic anatoa kila kitu kwa timu.Anakaba,anatuliza timu,anaendesha timu lakini pia anashambulia.Kubwa zaidi matic  ni mpambanaji mkubwa asiye choka.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video