Sunday, February 1, 2015

silva
VIGOGO wa England Manchester United, Liverpool, Everton, Tottenham wamechomoza na ushindi wa kuvutia na kuungana na timu za Newcastle United, Stoke City na Sunderland kutengeza ‘ Jumamosi isiyo na sare’. Wakati Chelsea itashuka Stamford Bridge kuwakabili mabingwa watetezi Manchester City ayari michezo saba imepigwa na yote imetoa washindi.

Katika mechi ya mapema, Newcastle ilichomoza na ushinsi wa mabao 3-0 katika uwanja wa The Kingstone Communications dhidi ya wenyeji Hull City. Remy Cabella alifunga bao la kuongoza kwa wageni dakika tano kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza, Sammy Ameobi akafunga lingine dakika tano baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, kabla ya  Yoan Gouffran kuitmishushindi wa ‘ The Toon’.

 Bao pekee kunako dakika ya pili lililofungwa na Romelo Lukaku lilitosha kuwapa ushindi wa kwanza ‘ Toffie’ baada ya michezo tisa. IKicheza uwanja wa nyumbani Selhurs Park, Crystal Palace ilishuhudia ikikubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa vijana hao wa Roberto Martinez, hiko ni kipigo cha kwanza kwa mkufunzi wa Palace, Alan Pardew.

Kijana anayeibeba Liverpool hivii  sasa, Rahem  Sterling aliwafungia ‘ Majogoo wa Anfield’ bao la kuongoza katika dakika ya 51 wakatI timu yake ya Liverpool ilipowashinda ‘ Wagonga nyundo wa London’ West Ham United kwa mabao 2-0. Mshambulizi Daniel Sturridge aliingia kuchukua nafasi ya Lazar Markovic katika dakika ya 68 na kucheza kwa mara ya kwanza baada ya kuwa nje kwa miezi mitatu. Mshambulizi huyo wa England aliwafungia Liverpool bao la pili zikiwa zimesalia dakika kumi mchezo kumalizika katika uwanja wa Anfield.

Manchester United imefanikiwa kulipa kisasi dhidi ya Leicester City kufuatia kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika uwanja wa Old Trafford. Robbin Van Persie na Radamel Falcao walifunga katika dakika za 27 na 32 kabla ya Wes Morgan kujifunga dakika ya 44 na kufanya vijana wa Luis Van Gaal kuwa mbele kwa mabao 3-0 kufikia nusu ya mchezo. Marcin Wasilewski aliwafungia wageni bao la kufutia machozi katika dakika ya mwisho ya mchezo.

Ikicheza katika uwanja wa nyumbani, Britania, Stoke City iliichapa QPR kwa mabao 3-1. Jonathan Walters alifunga mara mbili katika dakika za 21 na 24 kabla ya Niko  Kranjcar kuiwafungia wageni goli la kufutia machozi katika dakika ya 36. Walters alifunga ‘ hat-trick’ baada ya kuzamisha bao la tatu dakika ya mwisho ya mchezo.
 Mshambulizi Jermaine Defoe alifunga bao lake la kwanza tangu alipojiunga na Sunderland akitokea Toronto ya Marekani. ‘ Black Cats’ walichomoza na ushindi wa mabao 2-0 katika uwanja wa Stadium of Right dhidi ya  Burnley. Connor Wickham aliwafungia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 20 kabla ya Defoe kufunga lingine dakika 14 baadae.

IKicheza katika uwanja wa nyumbani The Hawthorns timu ya West Brom ilivurumishwa mabao 3-0 na Tottenham Hotspur.  Cristian Eriksen aliifungia Spurs bao la uongozi dakika ya 6 kabla ya Harry Kane kufunga mara mbili katika dakika za 15 na 64 alipofunga kwa mkwaju wa penalti.


Mchezo kati ya Chelsea na City ulimalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1, Loic Remy alitangulia kuwafungia wenyeji dakika ya 41 lakini kiungo msambulizi, David Silva akaisawazishia timu yake dakika ya mwisho kuelekea nusu ya kwanza ya mchezo huo .

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video