Wednesday, February 18, 2015



TIMU za African Sports ya Tanga na Mwadui FC ya Shinyanga zinatrajiwa kucheza mchezo wa fainali ya kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) siku ya jumamosi katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

 African Sports waliibuka washindi wa kwanza katika Kundi A, na Mwadui FC washindi wa kwanza Kundi B watacheza mchezo huo wa fainali ambapo Bingwa atapewa zawadi ya Kombe na medali, hali kadhalika kwa msindi wa pili.

 Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ilimalizika mwishoni mwa wiki kwa timu nne kupanda Ligi Kuu kwa kila kundi kutoa timu mbili, Kundi A ni African Sports na Majimaji FC, Kundi B ni timu za Mwadui FC na Toto Africans.

Baada ya kupokea taarifa hizo, kocha mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kwhelo ‘Julio’ ametamba kushinda mechi hiyo na kuwadhihirishia Watanzania kuwa yeye ni miongoni mwa makocha bora nchini.

Kwanza namshukuru Mungu mwingi wa rehema kwa kutuwezesha kucheza tena ligi kuu ya Vodacom, kumbuka mwaka jana tulipanda na kupata nafasi hiyo, lakini hatukuweza kucheza”. Amesema Julio na kuongeza : “ Mwaka huu tulijipanga upya na kuanza mchakato na hatima yake tumeweza kumaliza tena kwa kwanza katika kundi letu”.

Kuhusu mechi ya jumamosi, Julio amesema: “Tumepata taarifa kuwa tutacheza mchezo wa kutafuta bingwa wa jumla wa ligi daraja la kwanza, kwetu sisi tuko tayari na timu yangu inaondoka kwa basi maalumu kuja kucheza mechi hiyo siku ya jumamosi”.


“Tunataka kushinda mechi hiyo ili watu wajue kuwa Julio ni moja ya makocha bora nchini”

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video