Wednesday, February 18, 2015

KOCHA mkuu wa mabingwa wa zamani wa Tanzania mwaka 1988 waliofanikiwa kurejea tena ligi kuu soka Tanzania bara,  Africans Sports ya Tanga, Joseph Lazaro amefichua siri ya kapata mafanikio katika michuano ya ligi daraja ya kwanza iliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Africans Sports walimaliza vinara wa kundi A wakati Mwadui fc walimaliza wa kwanza kundi B, na timu hizo zitachuana jumamosi ya wiki hii uwanja wa Taifa, Dar es salaam kutafuta bingwa wa jumla wa ligi daraja la kwanza.

Akizungumza na mtandao huu, Lazaro amesema: “Siri ya kufanya vizuri kwangu ni kuwa karibu mno na wachezaji, kitu cha pili ni kujua malengo yetu. Wachezaji wangu na viongozi wangu tulikuwa na lengo la kupanda daraja”.


“Wachezaji ndio watakaokuangusha au kukubeba, lazima uwe karibu nao. Hivi nipo mazoezini, nakuja huko Dar es salaam, mimi naona kama ligi haijaisha. Nataka Nafasi ya kuwa bingwa wa makundi yote mawili”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video