
Wachezaji wa Ghana wakishangilia ushindi wao mbele ya kocha Avram Grant
NDOTO za Equatorial Guinea kutwaa ubingwa wa kombe la mataifa ya Africa, Afcon 2015 baada ya kufungwa mabao 3-0 na Ghana, lakini aibu kubwa imetawala baada ya mashabiki wa timu mwenyeji kufanya vurugu kubwa katika uwanja wa Malabo jana usiku na kusababisha mechi kusimama kwa dakika 35.
Wenyeji wameonesha kiwango kikubwa na maajabu makubwa katika michuano ya mwaka huu, lakini kutolewa hatua ya nusu fainali kuliwaudhi mashabiki ambao walirusha chupa kwa wachezaji wa Ghana, viongozi na mashabiki.

Wachezaji wakisubiri Helkopta iwatulize mashabiki ili mechi iendelee

Mashabiki wakificha nyuso zao wakati Helkopta inapita juu yao


Polisi wakipiga mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki waliokuwa wanafanya vurugu uwanja wa Malabo

Wachezaji wa Ghana wakitolewa chini ya ulinzi mkali

Shabiki wa Guinea ya Ikweta akiwa ametiwa mbaroni

Chupa za maji zikiwa zimesamba katika uwanja wa Malabo
0 comments:
Post a Comment