Martin Odegaard akipozi katika picha na jezi yake wakati alipotambulishwa Real Madrid
NYOTA kinda wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 16
aliyesajiliwa kwa paundi milioni 2.3, Martin Odegaard amethitibisha kuwa hamu ya kufanya kazi na Zinedine Zidane ndio imemfanya azipotezee timu za ligi kuu England na kujiunga na mabingwa hao wa Ulaya.
Kinda huyo wa Norwegian ambaye alitambulishwa katika uwanja wa klabu ya Real Madrid, atakuwa anapokea mshahara wa paundi elfu 40,000 kwa wiki katika msimu wake wa kwanza, lakini utaongezeka kutokana na Bonasi.
Amechagua Real Madrid licha ya kuzitembelea klabu za Liverpool na Arsenal wakati alipokuwa katika ziara ya kuziona timu kubwa barani ulaya.
Odegaard akipozi na wakali wa Real, Sergio Ramos (kushoto) na Cristiano Ronaldo baada ya kusaini jana alihamisi
Mkuregenzi wa Real, Emilio Butragueno alionekana kuwa na furaha kumkaribisha Odegaard mji mkuu wa Hispania
0 comments:
Post a Comment