MAAFANDE wa Ruvu Shooting wametamba kuifunga Yanga
katika mechi ya ligi kuu Tanzania bara itakayochezwa jumamosi uwanja wa Taifa
Dar es salaam na kufuta kipigo cha aibu
cha mabao 7-0 walichopata msimu uliopita.
Afisa bahari wa klabu hiyo, Masau Bwire amesema
Yanga walitamba kutwaa kombe la Mapinduzi, lakini walifungwa na timu ya JKU bao
1-0 na kutupwa nje hatua ya robo fainali.
‘Tunataka kuwaonesha Watanzania kuwa sisi sio timu
dhaifu, wanaitwa wazee wa wiki, tunataka kufuta aibu hiyo”
“Walitamba wanakwenda kuchukua kombe la Mapinduzi,
wamefungwa na kitimu kidogo cha JKU. Kwetu safari hii watatukoma”. Alisema
Masau.
0 comments:
Post a Comment