Saturday, January 17, 2015

Wanandinga wa Yanga wakifanya mazoezi jana uwanja wa Boko Veteran

YANGA SC imesema Ruvu Shootings watakayochuana nayo katika mchezo wa ligi kuu uwanja wa Taifa Dar es salaam haina uwezo wa kuifunga na usajili wake unaoishia Mlandizi tu.
Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro amesema usajili wa Yanga ni wa mamilioni, wanakwenda mpaka ulaya, Liberia, Rwanda na Burundi tofauti na Shootings wanaosajili mpaka Chalinze na Mlandizi.

“Kikosi bora kinaonekana bwana, sisi usajii wetu ni wa mamililioni, wenzetu usajili wao wa laki tano, wakisajili sana utakuta wamesajili kutoka Chalinze, utalinganisha na Yanga ambayo inasajili mpaka Ulaya”. Amesema Muro. “Tunafika Liberia, Burundi, Rwanda, utafananisha na timu inayosajili mwisho pale Mlandizi tu, mtutendee haki Yanga, Yanga ni timu kubwa”

Muro ameongeza kuwa Ruvu Shootings ni mtoto wao ambaye wanamlea na historia inawalinda kwani walishampa magoli 7-0.

“Alishapata magoli saba ya kutosha, tunacheza naye leo, hatuna wasiwasi kabisa, Yanga ni klabu bora na umri tuliokuwa nao hakuna mtu yeyote pale Ruvu Shootings mwenye umri kama wetu katika ligi”.


“Mkongwe ni mkongwe tu, hatuna wasiwasi, tuna wachezaji bora, benchi la ufundi bora, tumejipanga vizuri. Tunacheza mpira bora sio wa lamli moja jumlisha moja lazima iwe mbili, lazima tupate ushindi.” Aliongeza Muro.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video