Hans van der Pluijm (kushoto) na msaidizi wake Charles Boniface Mkwasa waliifunga Ruvu Shootings 7-0 msimu uliopita, je, watafanya nini kesho?
YANGA SC inawakaribisha maafande wa Ruvu Shootings
kutoka Pwani katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara itayopigwa kesho
uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Unapozitaja timu hizi mbili, kumbukumbu inayokuja
haraka kichwani ni kipigo cha 7-0 walichotoa Yanga msimu uliopita kwa wanajeshi
hawa wanaofundishwa na Tom Alex Olaba.
Kipigo hiki kilitolewa na kocha Hans van der
Pluijm na sasa amerejea tena na kukutana na Shootings katika mchezo wake wa
pili wa ligi kuu msimu huu.
Ikumbukwe kuwa desemba 28 mwaka huu, Yanga
walitoka sare ya mabao 2-2 na Azam fc na Pluijm alisema watafanya marekebisho
makubwa kabla ya kucheza mechi inayofuata ambayo ndio kesho.
Kipindi cha Marcio Maximo, Yanga ilikuwa inacheza
mpira wa kujilinda zaidi na mashabiki hawakufurahishwa na mfumo huo, lakini
ujio wa Pluijm umerejesha soka la kushambulia
zaidi.
Mliberia Kpah Sherman hakuwepo msimu uliopita, je, atafanya nini katika mechi yake ya pili ya ligi kuu?
Kocha huyu raia wa Uholanzi anacheza mpira wa
wazi, pasi za uhakika na kushambulia zaidi.
Wakiwa kombe la Mapinduzi, Yanga walishinda mabao
4-0 katika mechi mbili dhidi ya Polisi na Taifa ya Jang’ombe, ingawa walifungwa
bao 1-0 na JKU katika mechi ya robo fainali na kutupwa nje ya mashindano.
Mbali na kipigo hicho, Yanga walitengeneza nafasi
nyingi lakini Amisi Tambwe, Andrey Coutinho, Kpah Sherman, Mrisho Ngasa, Danny
Mrwanda na Saimon Msuva walishindwa kuzitumia.
Kutokana na kasi hiyo, Ruvu Shootings wanajiandaa
vikali kuhakikisha wanawazuia washambuliaji hatari wa Yanga.
Wapinzani wa Yanga, Ruvu Shootings ya Pwani
Msemaji wa klabu hiyo, Masau Bwire amesema Yanga sio timu ya kuogopwa, wamejipanga kufuta 7-0.
Wapinzani wa Yanga, Ruvu Shootings ya Pwani
Msemaji wa klabu hiyo, Masau Bwire amesema Yanga sio timu ya kuogopwa, wamejipanga kufuta 7-0.
“Wanajiita wazee wa nne nne, sijui wazee wa wiki,
tunataka kuwaonesha Watanzania kuwa timu yetu ina vijana wenye vipaji vya hali
ya juu, tunalipa zile 7-0”. Alisema Bwire mwenye maneno mengi mithiri ya
Chiriku.
Mechi nyingine za kesho ni Kagera Sugar dhidi ya
Mbeya City fc uwanja wa CCM Kirumba mwanza. Ndanda fc watakuwa wenyeji wa Simba
uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Stand United watawakaribisha Azam fc katika uwanja
wa CCM Kambarage mkoani Shinyanga, wakati Mgambo JKT watachuana na Tanzania
Prisons.
Jumapili, JKT Ruvu watacheza na Mtibwa Sugar
uwanja wa Azam Complex, Chamazi Dar es salaam na Coastal Union watachuana na
Polisi Morogoro uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.
0 comments:
Post a Comment