Kikosi cha Yanga kilichoanza leo
YANGA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika
michuano ya kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar kwenye uwanja wa
Amaan baada ya kuitandika mabao.. timu ya Polisi.
Mbrazil Andrey Coutinho alikuwa wa kwanza
kuiandikia Yanga bao la kuongoza katika dakika ya 27 ya kipindi cha kwanza na baadaye
dakika ya 33 Mliberia Kpha Sherman aliandika kimiani bao la pili akimalizia
mpira mzuri aliotengewa kwa njia ya kichwa na Amissi Tambwe.
Katika dakika ya 56 ya kipindi cha pili, Coutinho
aliandika bao la tatu kwa mpira wa adhabu ndogo.
Kikosi cha Polisi kilichoanza aleo
Katika day a 80 Saimon Msuva aliandika bao la nne
akimalizia pasi nzuri ya Salum Telela.
Hilo ni bao la nne la Msuva katika mechi mbili tu
za mashindano ya Mapinduzi 2015.
Huo ni ushindi wa pili kwa Yanga kwani katika
mechi ya kwanza iliyopigwa juzi uwanja wa Amaan, vijana hao wa Hans Van der
Pluijm waliitandika Taifa ya Jang’ombe mabao 4-0 ambapo Saimon Msuva alipiga
mabao matatu ‘hat-trick’ na moja
likifungwa na Sherman.
Yanga chini ya Pluijm wamebadilika kiuchezaji
ambapo wanashambulia zaidi tofauti na kipindi cha Marcio Maximo aliyekuwa
anatumia mbinu za kujihami zaidi.
Mbali na kushambulia, Yanga wanacheza mpira wa kupasiana
kwa dakika zote 90 na kupanga mashambulizi ya maana.
Baada ya mechi hii, majira ya saa 2:00 usiku,
mabingwa watetezi wa Tanzania bara, Azam fc watachuana vikali na KMKM ya
Zanzibar katika uwanja wa Amaan.
Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mechi mbili
kupigwa uwanja wa Amaan ambapo Mafunzo wataoneshana kazi na Mtibwa Sugar fc
majira ya saa 11:00 jioni na usiku saa 2:00, Simba watachuana na JKU.
0 comments:
Post a Comment